Wanafamilia
wa ABC Dental Centre inayomiliki na kuendesha ABC Dental Clinic wakiwa
katika picha ya pamoja mara walipofika katika Kituo cha kulelea watoto
wenye mahitaji Maalum kilichopo Chanika
Mmoja
wa wanafamilia Hassan akishusha vitu walivyoviandaa kwa ajili ya
misaada ya watoto wenye mahitaki maalum kwa lengo la kuwawezesha watoto
hao kufurahia na kujumuika na waumini wote Duniani katika kusherehekea
Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya kwa furaha
Wanafamilia hao wakijumuika na watoto hao kuiba wimbo kwa pamoja wa kuwakaribisha wageni
Mkurugenzi
na Mlezi wa ABC Dental Centre inayo miliki na kuendesha ABC Dental
Centre, Happy Kidata (wa tatu kulia) akimkabidhi Mratibu wa Kituo hicho,
Teddy Kimatare misaada mbalimbali yenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni
moja ikiwa ni kuadhimisha mwaka Mmoja tangu kuanzishwa ABC Nov, 2015, ,
wanafamilia wa ABC Dental Centre pamoja na marafiki na wadau wamshukuru
Mungu kwa kutowa Sadaka kwa kuwatembelea watoto wenye mahitaji Maalum
kwa kuwawezesha kwa kusherehekea Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya kwa
furaha
Mkurugenzi wa ABC Dental Clinic, Dokta. Gombo Felician (wa nne kulia) akisaidiana na Mkurugenzi na Mlezi wa ABC Dental Centre inayo miliki na kuendesha ABC Dental Centre, Happy Kidata (wa tatu kulia) kumkabidhi, Mratibu wa Kituo hicho, Teddy Kimatare ndoo ya mafuta ya kula
na alisema Dokta Gombo, Tumekuja kuwatembelea kwa kuwaletea zawadi
kigo kwa kuwaonyesha upendo kama tupo pamoja nanyi, tumewaletea zawadi
kwa ajili ya Sikukuu na zawadi hizo ni viatu vya watoto wa kike na
wakiume, kunanguo za watoto wa kike na watoto wa kiume, madaftari mengi,
kalamu za wino na penseli nyingi, mashuka mazuri kwa ajili ya vitanda
vyenu kwa watoto wa kike na watoto wa kikiume , sabuni zenye dawa za
kuogea za kuzuia upere na sabuni za kufulia pamoja na nguo za watoto
wakike na za wavulana na pia tumewaletea Sukari na mafuta ya kula
Mkurugenzi na Mlezi wa ABC Dental Centre inayo miliki na kuendesha ABC
Dental Centre, Happy Kidata (wa tatu kulia) akikadhidhi mfuko wa Sukari
kwa watoto hao pamoja na Mratibu wa Kituo hicho, Teddy Kimatare, (aliyevaa kitenge )
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa Kampuni ya KM Express Photo Studio na Mmiliki wa ujijirahaa blog
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269