Breaking News

Your Ad Spot

Dec 22, 2016

WAZIRI WA AFYA APOKEA NYUMBA 20 ZA WATUMISHI WA AFYA ZILIZOJENGWA NA TAASISI YA BENJAMINI MKAPA MKOANI MWANZA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (katikati), hii leo akikata utepe kuashiria upokeaji wa nyumba 20 mkoani Mwanza, zilizojengwa na Taasisi ya Benjamini Mkapa. Nyumba 10 zimejengwa katika wilaya ya Ukerewe na 10 katika wilaya ya Magu.
#BMGHabari
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (katikati), akikata utepe kuashiria upokeaji wa nyumba 20 mkoani Mwanza, zilizojengwa na Taasisi ya Benjamini Mkapa.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto), akimpongeza mmoja wa wauguzi wa afya katika Zahanati ya Kijiji cha Sese wilayani Magu baada ya kupata nyumba ya kuishi ikiwa ni miongoni mwa nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisalimiana na viongozi mbalimbali mkoani Mwanza, alipowasili katika Kijiji cha Sese wilayani Magu kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisalimiana na baadhi ya watumishi wa taasisi ya Benjamin Mkapa alipowasili katika Kijiji cha Sese wilayani Magu kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi hiyo mkoani Mwanza hii leo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akizungumza wakati wa halfa ya kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa, mkoani Mwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Khadija Nyembo akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati wa halfa ya kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa, mkoani Mwanza.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro, akizungumza wakati wa halfa ya kukabidhi nyumba 20 kwa Waziri wa Afya, zilizojengwa na taasisi hiyo mkoani Mwanza.
Baadhi ya watumishi wa taasisi ya Benjamin Mkapa wakijitambulisha kwenye halfa hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro (kushoto), akimkabidhi Waziri wa Afya, taarifa kuhusiana na ujenzi wa nyumba 20 za watumishi wa wizara hiyo zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo akiwemo mgeni rasmi, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, wakisaini vitabu vya wageni.
Diwani wa Kata ya Bujashi kilipo Kijiji cha Sese ambacho Zahanati yake imenufaika na nyumba hizo, akitoa shukurani zake kwa serikali.
Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure Kiswaga, akizungumza katika hafla hiyo ambapo lisha ya kuishukuru Wizara ya Afya kwa kwa kuendelea kuboresha huduma za afya. Amemuomba Waziri wa Afya kumsaidia upatikanaji wa gari la wagonjwa (Ambulance) katika vituo vya afya Kisesa na Ndagalu.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Sese wilayani Magu waliohudhuria halfa ya kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa, mkoani Mwanza.
Wapiga ngoza za asili kutoka Bujora wakitumbuizwa kwenye halfa hiyo
Wachezaji wa ngoza za asili kutoka Bujora wakitumbuizwa kwenye halfa hiyo ya kukabidhi nyumba 20 mkoani Mwanza, kwa waziri wa afya.
Waziri wa afya (wa tatu kushoto) pamoja na viongozi wengine wakicheza ngoma ya Kisukuma kutoka kwa akina mama wa Kijiji cha Sese wilayani Magu
Viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya zoezi la kupokea nyumba 20 za watumishi wa afya, zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza
Miongoni mwa nyumba 20 za watumishi wa afya, zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza
Baadhi ya watumishi wa Taasisi ya Benjamin Mkapa (wawili kushoto), wakitoa ufafanuzi wa jambo kwa wanahabari
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa tatu kulia), akiteta jambo na Mganga mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonald Subi (wa nne kulia), katika Kijiji cha Sese wilayani Magu, ilipofanyika hafla ya upokeaji wa nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amepokea nyumba ishirini kwa ajili ya watumishi wa afya katika wilaya za Magu na Ukerewe mkoani Mwanza, zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.

Nyumba hizo ni miongoni mwa nyumba 480 zinazojengwa na taasisi hiyo katika halmashauri 51 nchini tangu mwaka 2011, kupitia ufadhiri wa mfuko wa dunia wa kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu pamoja na Malaria wa Global Fund.

Akizungumza kwenye hafla ya kupokea nyumba hizo iliyofanyika katika Kijiji cha Sese wilayani Magu, Waziri Mwalimu, amesema serikali itaendelea kuboresha nyumba za watumishi wa afya nchini hususani wanaofanya kazi maeneo ya Vijijini.

“Nyumba hizi ni kwa ajili ya watumishi wa afya, hatutavumilia kuona anakaa mtu ambaye siyo mtumishi wa sekta hiyo. Tunataka kuvutia watumishi wa afya kwenda vijijini ikiwemo mwaka huu ambapo pia tunataka tuwe na nyumba za vyumba vitatu ili mtumishi ambaye hajaoa apate vyumba yenye vyumba viwili na aliyeoa apate nyumba yenye vyumba vitatu”. Amesisitiza Mwalimu.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro, amebainisha kwamba nyumba hizo zimegharibu zaidi ya shilingi Bilioni moja ambapo kila nyumba yenye baraza, sebule, vyumba vitatu vya kulala, jiko, uzio, mfumo wa kuvuna maji wenye tenki la lita 3,000, choo, bafu pamoja na mfumo wa umeme imegharimu wastani wa shilingi Milioni 51. Nyumba hizo zimejengwa na Kampuni ya Grinda Builders & Supplies.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Magu, Khadija Nyembo, amesema huduma za afya zimeendelea kuboreshwa mkoani Mwanza ambapo kuna vituo vya kutoa huduma za afya 388  ambapo Zahanati ni 301, Vituo vya afya 53 na Hospitali 17 na kwamba halimashauri zote zinaendelea kuhamasishwa ili kuendelea kuongeza idadi ya vituo vya afya ili kufikia lengo la kuwa na Zahanati kila Kijiji, Kituo cha afya kila Kata na Hospitali kila Wilaya.

Kwa mjibu wa Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonald Subi, mkoa wa Mwanza una nyumba za watumishi wa afya zipatazo 347 ambapo bado kuna upungufu wa nyumba 661 ili kusaidia watumishi wa sekta hiyo kuishi karibu na vituo vyao vya kazi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages