Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
(katikati), hii leo akikata utepe kuashiria upokeaji wa nyumba 20 mkoani
Mwanza, zilizojengwa na Taasisi ya Benjamini Mkapa. Nyumba 10
zimejengwa katika wilaya ya Ukerewe na 10 katika wilaya ya Magu.
#BMGHabari
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (katikati),
akikata utepe kuashiria upokeaji wa nyumba 20 mkoani Mwanza,
zilizojengwa na Taasisi ya Benjamini Mkapa.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto),
akimpongeza mmoja wa wauguzi wa afya katika Zahanati ya Kijiji cha Sese
wilayani Magu baada ya kupata nyumba ya kuishi ikiwa ni miongoni mwa
nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisalimiana
na viongozi mbalimbali mkoani Mwanza, alipowasili katika Kijiji cha Sese
wilayani Magu kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin
Mkapa.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisalimiana
na baadhi ya watumishi wa taasisi ya Benjamin Mkapa alipowasili katika
Kijiji cha Sese wilayani Magu kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi
hiyo mkoani Mwanza hii leo.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akizungumza
wakati wa halfa ya kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin
Mkapa, mkoani Mwanza.
Mkuu wa Wilaya ya
Magu, Khadija Nyembo akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
wakati wa halfa ya kupokea nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin
Mkapa, mkoani Mwanza.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya
Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro, akizungumza wakati wa halfa ya
kukabidhi nyumba 20 kwa Waziri wa Afya, zilizojengwa na taasisi hiyo
mkoani Mwanza.
Baadhi ya watumishi wa taasisi ya Benjamin Mkapa wakijitambulisha kwenye halfa hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya
Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro (kushoto), akimkabidhi Waziri wa
Afya, taarifa kuhusiana na ujenzi wa nyumba 20 za watumishi wa wizara
hiyo zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo akiwemo mgeni rasmi, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, wakisaini vitabu vya wageni.
Diwani wa Kata ya Bujashi kilipo Kijiji
cha Sese ambacho Zahanati yake imenufaika na nyumba hizo, akitoa
shukurani zake kwa serikali.
Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure
Kiswaga, akizungumza katika hafla hiyo ambapo lisha ya kuishukuru Wizara
ya Afya kwa kwa kuendelea kuboresha huduma za afya. Amemuomba Waziri wa
Afya kumsaidia upatikanaji wa gari la wagonjwa (Ambulance) katika vituo
vya afya Kisesa na Ndagalu.
Baadhi ya wakazi wa
Kijiji cha Sese wilayani Magu waliohudhuria halfa ya kupokea nyumba 20
zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa, mkoani Mwanza.
Wapiga ngoza za asili kutoka Bujora wakitumbuizwa kwenye halfa hiyo
Wachezaji wa ngoza za asili kutoka
Bujora wakitumbuizwa kwenye halfa hiyo ya kukabidhi nyumba 20 mkoani
Mwanza, kwa waziri wa afya.
Waziri wa afya (wa tatu kushoto) pamoja
na viongozi wengine wakicheza ngoma ya Kisukuma kutoka kwa akina mama wa
Kijiji cha Sese wilayani Magu
Viongozi mbalimbali wakiwa katika picha
ya pamoja baada ya zoezi la kupokea nyumba 20 za watumishi wa afya,
zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza
Miongoni mwa nyumba 20 za watumishi wa afya, zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani Mwanza
Baadhi ya watumishi wa Taasisi ya Benjamin Mkapa (wawili kushoto), wakitoa ufafanuzi wa jambo kwa wanahabari
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa tatu
kulia), akiteta jambo na Mganga mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonald Subi (wa
nne kulia), katika Kijiji cha Sese wilayani Magu, ilipofanyika hafla ya
upokeaji wa nyumba 20 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa mkoani
Mwanza.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amepokea
nyumba ishirini kwa ajili ya watumishi wa afya katika wilaya za Magu na
Ukerewe mkoani Mwanza, zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.
Nyumba hizo ni
miongoni mwa nyumba 480 zinazojengwa na taasisi hiyo katika halmashauri
51 nchini tangu mwaka 2011, kupitia ufadhiri wa mfuko wa dunia wa
kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu pamoja na Malaria wa Global Fund.
Akizungumza
kwenye hafla ya kupokea nyumba hizo iliyofanyika katika Kijiji cha Sese
wilayani Magu, Waziri Mwalimu, amesema serikali itaendelea kuboresha
nyumba za watumishi wa afya nchini hususani wanaofanya kazi maeneo ya
Vijijini.
“Nyumba hizi ni
kwa ajili ya watumishi wa afya, hatutavumilia kuona anakaa mtu ambaye
siyo mtumishi wa sekta hiyo. Tunataka kuvutia watumishi wa afya kwenda
vijijini ikiwemo mwaka huu ambapo pia tunataka tuwe na nyumba za vyumba
vitatu ili mtumishi ambaye hajaoa apate vyumba yenye vyumba viwili na
aliyeoa apate nyumba yenye vyumba vitatu”. Amesisitiza Mwalimu.
Afisa Mtendaji
Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa, Dkt.Hellen Senkoro, amebainisha
kwamba nyumba hizo zimegharibu zaidi ya shilingi Bilioni moja ambapo
kila nyumba yenye baraza, sebule, vyumba vitatu vya kulala, jiko, uzio,
mfumo wa kuvuna maji wenye tenki la lita 3,000, choo, bafu pamoja na
mfumo wa umeme imegharimu wastani wa shilingi Milioni 51. Nyumba hizo
zimejengwa na Kampuni ya Grinda Builders & Supplies.
Akizungumza kwa
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Magu, Khadija
Nyembo, amesema huduma za afya zimeendelea kuboreshwa mkoani Mwanza
ambapo kuna vituo vya kutoa huduma za afya 388 ambapo Zahanati ni 301,
Vituo vya afya 53 na Hospitali 17 na kwamba halimashauri zote
zinaendelea kuhamasishwa ili kuendelea kuongeza idadi ya vituo vya afya
ili kufikia lengo la kuwa na Zahanati kila Kijiji, Kituo cha afya kila
Kata na Hospitali kila Wilaya.
Kwa mjibu wa
Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonald Subi, mkoa wa Mwanza una nyumba
za watumishi wa afya zipatazo 347 ambapo bado kuna upungufu wa nyumba
661 ili kusaidia watumishi wa sekta hiyo kuishi karibu na vituo vyao vya
kazi.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269