Kikosi cha Yanga SC leo dhidi ya JKT Ruvu FC
Kikosi cha JKT Ruvu SC leo dhidi ya Yanga FC
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
MABINGWA
watetezi wa ligi kuu Vodacom Yanga imefanikiwa kupanda hadi kileleni mwa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi
ya JKT Ruvu jioni ya leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Kwa
ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 36 baada ya kucheza mechi 16 na
kuishusha Simba iliyomalizia kileleni mzunguko wa kwanza kwa pointi zake
35.
Winga
Simon Msuva aliweza kuwa nyota wa mchezo huio baada ya kufanikiwa
kuifungia timu yake goli mbili katika dakika ya 57 na 90 huku lingine
akipiga pande safi linalomshinda beki Michael Aidan na kuingia nao
nyavuni dakika ya 38.
JKT Ruvu
waliweza kucheza kandanda safi na wakionekana kutumia mashuti ya mbali
kuweza kujaribu nafasi ya kufunga huku mshambuliaji wake Atupele Green
akikosa nafasi mbili za wazi.
Mkurugenzi
wa Ufundi wa Yanga, Mholanzi Hans van der Pluijm alikuwepo jukwaa kuu
kufuatilia mchezo, wakati kiungo mpya kutoka Zambia, Justin Zulu pia
akiwa jukwaani kwa sababu bado hajapatiwa kibali cha kufanya kazi
nchini.
Baada ya
mchezo, kocha msaidizi Juma Mwambusi amesema kuwa waliingia uwanjani na
mpango wakushinda na wamefaniklisha hilo ingawa mchezo ulikuwa mgumu
sana kwao.
Mechi hiyo ilichezeshwa na Hery Sasii akisaidiwa na Hellen Mduma na Kassim Mpanga wote wa Dar es Salaam.
Matokeo mengine ni:
Mwadui
1-0 Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Mbeya City 0-0 Kagera
Sugar Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Ruvu Shooting 1-1 Mtibwa Sugar Uwanja
wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.
Kikosi cha Yanga kilikuwa;
Deo
Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Haruna Niyonzima, Mwinyi Hajji Mngwali,
Kelvin Yondan, Vincent Bossou, Simon Msuva, Thabani Kamusoko/Geoffrey
Mwashiuya dk84, Donald Ngoma, Amissi Tambwe/Said Juma ‘Makapu’ dk55na
Deus Kaseke/Obrey Chirwa dk90
JKT Ruvu:
Hamisi Seif, Michael Aidan, Edward Charles, Yussuf Chuma, Kelvin
Nashon/Naftal Nasho dk66, Rahim Juma, Ally Bilal/Mussa Juma dk77, Hassan
Dilunga, Najim Magulu, Atupele Green/Saad Kipanga dk77 na Edward
Joseph.
Mshambuliaji
wa Yanga SC,Deus Kaseke (katikati) akiwatoka mabeki wa timu ya JKT Ruvu
leo katika uwanja wa Uhuru mchezo uliomaizika kwa Yanga SC kuibuka na
ushindsi wa goli 3-0 leo jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji
wa timu ya JKT Ruvu ,Naftal Nashon (wakwanza kulia) akimtoka beki wa
timu ya Yanga leo katika uwanja wa Uhuru mchezo uliomaizika kwa Yanga SC
kuibuka na ushindsi wa goli 3-0 leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa
Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba akijadiliana jambo na Mbunge wa
Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa mechi ya ligi kuu kati ya JKT Ruvu
na Yanga leo Jijini Dar es salaam.
Kiungo mpya kutoka Zambia, Justin Zulu (katikati) akiwa jukwaani kwa sababu bado hajapatiwa kibali cha kufanya kazi nchini.
Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269