Breaking News

Your Ad Spot

Jan 14, 2017

AU YATISHIA HATUA KALI DHIDI YA YAHYA JAMMEY

Rais Yahya Jammeh wa Gambia
Rais Yahya Jammeh wa Gambia
Muungano wa Afrika AU umesema kuwa utawacha kumtambua Yahya Jammeh kama rais wa Gabon kuanzia tarehe 19 Januari wakati muda wake utakapokamilika.
Baraza la amani na usalama la muungano huo pia limetishia kuchukua hatua kali iwapo vitendo vya Jammeh vitasababisha mauaji ya raia wasio na hatia.
Muungano huo pia umevitaka vikosi vyake vya kulinda amani kujizuia.
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari yuko nchini Gambia akiongoza ujumbe wa mataifa ya magharibi ECOWAS katika jaribio la hivi karibuni kumshawishi bwana Jammeh kuwachilia mamlaka kwa Adama Barrow ambaye alishinda uchaguzi wa urais mwezi uliopita.
Adama Barrow na Yahya Jammeh
Adama Barrow na Yahya Jammeh
Bwana Barrow ameambia BBC kwamba ataapishwa kama rais wiki ijayo na kumtaka Jammeh ashiriki katika mazungumzo na wapatanishi hao.
Aidha memtaka Rais anayemaliza muda wake Yahya Jammeh kushiriki katika mazungumzo ya moja kwa moja ili kutatua mgogoro wa kisiasa ulioikumba nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages