Breaking News

Your Ad Spot

Jan 17, 2017

BURUNDI YAANZA KUONDOA ASKARI WAKE WA KULINDA AMANI SOMALIA

Serikali ya Burundi imeanza kuwaondoa wanajeshi wake wanaohudumu katika Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom kutokana na mgogoro wa mshahara.
Gaston Sindimwo, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi amesema kuwa, serikali ya Bujumbura imeamua kutekeleza maamuzi hayo magumu kutokana na kutotiliwa maanani ombi lake la kutaka kadhia ya mishahara na marupurupu ya wanajeshi wake walioko Somalia itatuliwe haraka iwezekanavyo. Sindimwo amenukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa: "Tungependa kuendelea kusaidia mchakato wa kurejesha amani na uthabiti nchini Somalia, lakini tunalazimika kuanza kuwaondoa askari wetu kwa kuwa hawajalipwa mishahara na marupurupu yao kwa zaidi ya miezi 12 sasa."
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi ambaye mwezi uliopita alitishia kuwaondoa wanajeshi wa nchi yake walioko Somalia iwapo askari hao hawangelipwa mishahara yao kufikia mwezi huu, sasa amewaagiza mawaziri wa mambo ya nje na ulinzi wa nchi hiyo kuanzisha mchakato wa kuwaondoa wanajeshi wa nchi hiyo Somalia. Mwishoni mwa mwezi uliopita wa Disemba, Rais Nkurunziza alisema nchi hiyo itaushtaki Umoja wa Afrika katika vyombo vya mahakama vya kimataifa kwa kukiuka muafaka uliofikiwa na pande zote kuhusiana na mishahara ya askari wa Amisom.
Burundi ambayo ina askari 5,432 ndani ya Amisom, ni nchi ya pili baada ya Uganda kwa kuwa na idadi kubwa ya askari wa kulinda amani nchini Somalia. Kikosi hicho kimetumwa Somalia lengo likiwa ni kuendesha mapambano ya kulitokomeza kundi la kigaidi la wanamgambo wa al Shabab ambalo linataka kuipindua serikali kuu ya Somalia. 
Wanajeshi wa Burundi nchini Somalia
Amisom ilijikuta katika kipindi kigumu cha kuwalipa mishahara wanajeshi zaidi ya 22 elfu wa nchi za Afrika zilizotuma askari wake Somalia zikiwa ni pamoja na Kenya, Ethiopia na Djibouti, baada ya Umoja wa Ulaya EU kupunguza bajeti yake kwa kikosi hicho cha kulinda amani, kwa asilimia 20 mapema mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages