Meneja
Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar Abdalla Suleiman Ali akifungua
mkutano wa siku moja wa wadau wa Malaria uliofanyika Hoteli ya Ocean
View Kilimani Mjini Zanzibar.
Afisa
uchunguzi wa vimelea vya Malaria Zanzibar Safia Mohammed Ali
akiwasilisha mada ya njia za kukabiliana na maradhi hayo katika mkutano
wa wadau wa Malaria uliofanyika Hoteli ya Ocean View Kilimani .
Naibu
Meneja wa ZAMEP Faiza Bwanakheri akitoa mada ya njia za kudhjibiti na
kumaliza Malaria Zanzibar katika mkutano wa wadau wa Malaria uliofanyika
Hoteli ya Ocean View.
Baadhi ya
wadau wa Malaria walioshiriki mkutano wa siku moja katika Hoteli ya
Ocean View wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano
huo.(Picha na Makame Mshenga).
Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar
Meneja
Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar Abdalla Suleiman Ali amesema
mashirikiano ya pamoja yanahitajika kuanzia ngazi ya shehia hadi Taifa
katika kufikia malengo ya kumaliza maradhi hayo nchini.
Alisema
kazi ya kumaliza Malaria Zanzibar sio kazi rahisi kama inavyofikiriwa
na watu wengi lakini nguvu za pamoja za wadau mbali mbali wa ndani na
nje ya nchi zinahitajika.
Meneja
Abdalla Suleiman alieleza hayo katika mkutano wa siku moja wa wadau wa
Malaria uliozungumzia hali ya ugonjwa huo ulivyo hivi sasa na juhudi
zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali kupitia kitengo hicho uliofanyika
Hoteli ya Ocean View Kilimani Mjini Zanzibar.
Alisema
pamoja na Zanzibar kupata mafanikio makubwa katika kukabiliana na
Malaria bado zipo baadhi ya sehemu maradhi hayo yanaendelea kujitokeza
na ni vigumu kukabiliana nayo kwa vile kunahitajika ufuatiliaji wa
karibu kwenye familia zinazotoka wagonjwa hao.
Aliongeza
kuwa kabla ya kuanzishwa kitengo cha kumaliza Malaria, Zanzibar
ilifikia kuwa na wagonjwa zaidi ya laki tatu kwa mwaka lakini hivi
sasa wagonjwa wa malaria hawazidi elfu nne kwa mwaka.
Alisisitiza
kuwa lengo la Wizara ya Afya kupitia Kitengo cha kumaliza Malaria ni
kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2022 Zanzibar hakuna mtu anaeugua
Malaria.
Akitoa
mada ya hali ya Malaria ilivyo hivi sasa, Ofisa wa Kitengo hicho Wahida
Shirazi alisema Kisiwa cha Unguja kunawagonjwa wengi zaidi wa maradhi
hayo ukilinganisha na Pemba na Wilaya ya Kati inaongoza kwa wagonjwa
wengi ikifuatiwa na Wilaya za Magharibi.
Alikumbusha
kuwa Wilaya ya Chake Chake inaongoza kwa kuwa na wagonjwa kidogo zaidi
wa Malaria na baadhi ya shehia za Wilaya hiyo hazijatoa mgonjwa hata
mmoja kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Hata
hivyo Ofisa huyo alisema Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar
kimegundua wagonjwa wengi wa malaria hivi sasa ni wenye tabia ya
kusafiri mara kwa mara nje ya Zanzibar na wanaamini wanapata ugonjwa huo
wakati wa safari zao.
Akizungumzia
umuhimu wa kutumia vyandarua katika kupambana na Malari Afisa wa
Kitengo hicho Mwinyi Khamis alisema iwapo vitatumika vizuri vinaepusha
maradhi hayo kwa asilimia sitini hivyo amewashauri wananchi kuendelea
kuvitumia kikamilifu.
Baadhi ya
wadau walioshiriki mkutano huo walikishauri kitengo cha kumaliza
mlaria kutoa elimu zaidi kwa wananchi wanaokataa nyumba zao kupigiwa
dawa badala ya kuviachia vyombo vya dola kutumia nguvu kukamililsha kazi
hiyo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269