Breaking News

Your Ad Spot

Jan 19, 2017

MGOGORO WA GAMBIA WAINGIA SURA MPYA, NIGERIA YATUMA MAJESHI KUKABILIANA NA JAMMEH

Yahya Jammeh
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limetuma askari 200 na ndege kadhaa za kivita katika nchi jirani na Gambia ya  Senegal kwa ajili ya kutatua mgogorowa uongozi uliosababishwa na uchaguzi wa rais nchini Gambia.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Anga la Nigeria imesema kuwa, kundi la askari 200, ndege kadhaa za kivita, manuari ya kijeshi, helikopta na ndege za ujasusi zimepelekwa nchini Senegal kwa ajili ya kufuatilia hali ya mambo nchinI Gambia.
Hatua hiyo imechukuliwa huku nchi za Magharibi mwa Afrika zikijitayarisha kutuma majeshi nchini Gambia kwa ajili ya kumuondoa madarakani kwa nguvu Bwana Yahya Jammeh ambaye kipindi chake cha uongozi kinamalizika leo. 

Senegal pia imetangaza kuwa iwapo Yahya Jammeh atang'ang'ang'ania madaraka jeshi la nchi hiyo liko tayari kuingia nchini humo na kurejesha utawala wa kisheria.

Yahya Jammeh ambaye alishindwa na Adama Barrow katika uchaguzi wa rais wa Gambia anapaswa kukabidhi madaraka ya nchi hii leo tarehe 19 Januari.
Wakati huo huo, mamia ya wananchi wa Gambia wameanza kuondoka nchini humo wakikimbilia usalama wao katika nchi jirani. 

Thomas Cook, afisa wa masuala ya utalii raia wa Uingereza amesema wameanza kuondoa watalii1000 hii leo huku wengine 2,500 wakitazamiwa kuondolea nchini humo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages