Breaking News

Your Ad Spot

Jan 14, 2017

MILIO YA RISASI YASIKIKA KATIKA MJI ULIOKUMBWA NA MACHAFUKO WA BOUAKE, COTE D'LVOIRE

Milio ya risasi imesikika katika mji uliokumbwa na hali ya mchafukoge wa Bouaké, huko kaskazini mwa Côte d’Ivoire.
Ufyatuaji risasi huo umetokea katika hali ambayo mazungumzo ya siku mbili baina ya Alain Richard Donwaki Waziri wa Uulinzi na askari waasi yangali yanaendelea mjini hapo. Kwa mujibu wa mashuhuda, risasi zimesikika karibu na kituo cha utamaduni ambako imepangwa kuwa Richard Donwaki na kiongozi wa askari hao waasi watakutana kwa ajili ya mazungumzo hayo.
Askari waasi nchini Côte d’Ivoire
Wakati huo huo, askari waliopo katika mji wa Daloa katikati mwa Côte d’Ivoire wamefyatua risasi angani suala ambalo limewafanya wafanyabiashara wa mji huo kufunga maduka yao kwa kuhofia usalama wao. Uasi wa askari nchini Côte d’Ivoire uliibuka tarehe sita mwezi huu katika mji wa Bouaké na kusambaa haraka katika miji mingine ya Ivory Coast ukiwemo mji wa kiuchumi wa Abidjan. Hii ni katika hali ambayo serikali ya Yamoussoukro, imeahidi kutekeleza matakwa ya askari hao ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara yao, kuwalipia bima na makazi.
Baadhi ya askari waasi
Kufuatia uasi huo, Rais Alassane Ouattara aliwapiga kalamu nyekundu makamanda wa jeshi na polisi nchini humo. Kwa mujibu wa weledi wa mambo machafuko hayo mapya yatazorotesha juhudi za rais huyo za kujaribu kutuliza hali ya mambo nchini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages