Rais mteule wa Marekani Donald Trump wakati wa mkutano na vyombo vya habari, mjini New York, Januari 11, 2017.
Rais
mteule wa Marekani Donald Trump atakayechukua hatamu ya uongozi wa nchi
Januari 20 amekutana kwa mara yake ya kwanza na waandishi
wa habari tangu achaguliwe Novemba 8.
Akionekana
ni mwenye hasira dhidi ya vyombo vya habari, rais mteule wa Marekani
amezungumzia masuala mbalimbali kama vile mahusiano yake na Urusi,
kurejelea upya sera ya Obamacare, na mpango wake wa kujenga ukuta na
Mexico.
Rais
mteule wa Marekani Donald Trump ameshutumu tangu mwanzo wa mkutano wake
na waandishi wa habari, taarifa za uongo zilizosambazwa katika baadhi ya
vyombo vya habari nchini Marekani kuhusu mahusiano yake na Urusi.
Mahusiano na Putin
Rais
mteule wa Marekani pia amesema hakujua kama angeweza kuelewana na Putin
lakini ana matumaini kuwa itakuwa hivyo. Bilionea huyo kutoka chama cha
Republican anasema ni "jambo muhimu" kuona rais wa Urusi anakuwa upande
wake. "Kama Putin anampenda Trump, ni vizuri, si tatizo lolote," amesema
Bw Trump.
Trump aachana na kazi ya biashara
Rais
mteule wa Marekani Donald Trump pia ametangaza kukata mahusiano na
shughuli zake nyingi za kibiashara na kifedha kwa kuhamisha mali yake
yote katika kampuni ya "Trust" inayosimamiwa na wanawe wawili.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269