Jared Kushner na mke wake.
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amemteua mkwe wake Jared Kushner, kuwa mshauri mwandamizi wa Ikulu ya nchi hiyo.
Kushner
mwenye umri wa miaka 35 ambaye amemuoa binti mkubwa wa Trump, Ivanka,
alifanya kazi kubwa wakati wa kampeni za uchaguzi, zilizomuwezesha Trump
kushinda.
Majukumu
ya kazi yake yanatarajiwa kuhusika na masuala ya sera za nje na ndani ya
nchi, ikiwemo masuala ya biashara na Mashariki ya Kati.
Uteuzi huo hauhitaji kuthibitishwa na bunge la seneti.
Lakini hata hivyo baadhi ya wachambuzi wanahoji kama uteuzi huo utakiuka sheria ya kupinga upendeleo wa undugu katika ajira.
Jared
Kushner hata chukua mshahara kwa uteuzi huo wa Ikulu ya Marekani na
itampa nafasi ya kumfanya kuwa huru na maslahi ya shughuli zake za
kibiashara
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269