Breaking News

Your Ad Spot

Jan 14, 2017

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MWIGULU NCHEMBA AFUNGA RASMI MAFUNZO YA KIKOSI MAALUM CHA MAGEREZA JIJINI DAR

 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimvisha nembo ya kijani Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kwa niaba ya wahitimu wenzake. Mafunzo hayo Maalum yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akitoa hotuba fupi kwa Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kabla ya kuyafunga rasmi leo Januari 13, 2017.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufunga Mafunzo hayo.
Askari Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 wakiingia uwanjani kwa ajili ya kutoa maonesho mbalimbali ya Ukakamavu na ujasiri.
Onesho Maalum la Ukakamavu na ujasiri kama inavyoonekana katika picha Askari wa Kikosi Maalum akihimiri kipigo cha nyundo katika mwili wake kwa ujasiri wa hali ya juu.
Askari Wahitimu wa Mafunzo hayo Maalum wakionesha umahiri wao wa kuvuka vikwazo mbalimbali kwa kutumia kamba kama inavyoonekana katika picha.
Wahitimu wa Mafunzo Maalum wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mgeni rasmi kama inavyoonekana katika picha(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akipokea Salaam ya heshima kutoka Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11. Hafla ya hiyo imefanyika leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam(kushoto) ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Dkt. Juma Malewa .
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akikagua Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na Askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kama inavyoonekana katika picha.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimtunuku cheti cha sifa Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 ambapo Mafunzo hayo yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages