Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimvisha nembo ya
kijani Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha
Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kwa niaba ya wahitimu wenzake. Mafunzo
hayo Maalum yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya
Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini
Dar es Salaam.
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akitoa hotuba fupi kwa
Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi
Namba 11 kabla ya kuyafunga rasmi leo Januari 13, 2017.
Kaimu
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa
maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufunga Mafunzo hayo.
Askari
Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi
Namba 11 wakiingia uwanjani kwa ajili ya kutoa maonesho mbalimbali ya
Ukakamavu na ujasiri.
Onesho
Maalum la Ukakamavu na ujasiri kama inavyoonekana katika picha Askari wa
Kikosi Maalum akihimiri kipigo cha nyundo katika mwili wake kwa ujasiri
wa hali ya juu.
Askari
Wahitimu wa Mafunzo hayo Maalum wakionesha umahiri wao wa kuvuka vikwazo
mbalimbali kwa kutumia kamba kama inavyoonekana katika picha.
Wahitimu
wa Mafunzo Maalum wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mgeni rasmi kama
inavyoonekana katika picha(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akipokea Salaam ya
heshima kutoka Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na askari
wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi
Namba 11. Hafla ya hiyo imefanyika leo Januari 13, 2017 katika Viwanja
vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga,
Jijini Dar es Salaam(kushoto) ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo
Dkt. Juma Malewa .
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akikagua Gwaride
Maalum la heshima lililoandaliwa na Askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya
Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kama inavyoonekana
katika picha.
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimtunuku cheti cha
sifa Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha
Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 ambapo Mafunzo hayo yamefungwa rasmi leo
Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia
Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269