Breaking News

Your Ad Spot

Jan 27, 2017

ZIARA YA NAIBU WAZIRI MASAUNI ATEMBELEA IDARA ZILIZOPO CHINI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI MKOANI MBEYA

Naibu Waziri wa Wizar ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelote Stephen mara baada ya kumaliza kupokea taarifa ya mkoa na taarifa ya vyombo vya usalama mkoa huo wakati wa ziara ya kikazi mkoani hapo. (PICHA NA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI)
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelote Stephen akitoa taarifa ya mkoa na taarifa ya vyombo vya usalama  mkoa huo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani  ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), wakati wa ziara ya Naibu Waziri kutembelea idara zilizopo chini ya wizara yake.
Naibu Waziri wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza mkoa wa Rukwa kwa ziara ya kikazi, Kulia ni wakuu wa jeshi hilo mkoani hapo  wakimsikiliza.
Afisa Uhamiaji Mkoa wa  Rukwa, Kamishna Msaidizi Selemani Kameya akisoma taarifa ya utendaji kazi ya Mkoa huo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, ACP George Kyando akizungumzia Mradi wa Ujenzi wa ofisi wakati Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya mradi huo na kuwataka kutumia rasilimali watu ya wafungwa waliopo mkoani hapo ili kuweza kukamilisha ujenzi huo wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya mkoani hapo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akipokea risala kutoka kwa askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Rukwa mara baada ya  kuisoma kwa niaba ya wenzake ikiwa na maombi mbalimbali yaliyoelekezwa kwa wizara.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana na aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simiyu, Paul Mzindakaya baada ya kumaliza kupokea taarifa ya hali ya usalama mkoani Rukwa wakati Naibu Waziri alipokuwa mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages