Breaking News

Your Ad Spot

Feb 14, 2017

WAZIRI UMMY ATEMBELEA HOSPITALI YA RUFAA TEMEKE

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea wodi ya watoto wachanga katika hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam ili kujionea vifaa tiba kwa ajili ya kuokoa maisha ya vichanga. Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 vilitolewa na CCBRT kwa hospitali za Mwananyamala, Amana, Temeke na hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ufadhili wa Taasisi ya Vodafone kupitia ubia wake na USAID/PEPFAR.
 Mshauli wa kiufundi wa mradi wa kujenga uwezo afya ya uzazi mama na mtoto wa CCBRT Dk. Brenda D'mello (kushoto) akizungumza jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati alipotembelea wodi za akimama katika  Hospitali ya Temeke Jijini, Dar es Salaam jana hafla ya kukabidhiwa vifaa Tiba vya Afya ya Uzazi vilivyo fadhiliwa na CCBRT
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Hospitalini hapo, wakwanza kushoto ni Mganga Mkuu Manispaa ya Temeke, Dk. Gwamaka Mwabulambo na kulia ni mshauri wa sekta ya afya na kiongozi wa timu katika masuala ya kimataifa canada na mambo ya nje Canada, Madani Thiam
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto kutoka CCBRT Dk, Mchomvu Francis (wapili kulia) akimwelezea jambo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) wakati alipotembelea Hospitali ya Rufaa Temeke Dar es Salaam jana katika Wod ya watoto wakati wa hafla kukabidhi vifaa Tiba vya Afya ya Uzazi vilivyo fadhiliwa na CCBRT. ambapo Dk Mchomvu na timu ya wataalamu wengine kutoka CCBRT mara nyingi hufanya kazi katika vituo na hospitali za serikali zenye ubia na CCBRT ili kutoa ujuzi wao kwa wahudumu wa afya wa Serikali.

 Sehemu ya wafanyakazi kutoka Idara mbalimbali
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) akizungumza jambo na mshauri wa sekta ya afya na kiongozi wa timu katika masuala ya kimataifa canada na mambo ya nje Canada, Madani Thiam wa pili kulia na  Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Erwin Telemans wa kwanza  kulia mara alipotembelea Hospitali ya Rufaa Temeke Dar es Salaam jana katika Wod ya watoto katika hafla kukabidhi vifaa Tiba vya Afya ya Uzazi vilivyo fadhiliwa na CCBRT.
  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia) akizungumza na Mwanaharusi Muhamed mara alipofika katika wod ya akinamama ambaye amelazwa hospitalini hapo
  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kushoto waliokaa) akizungumza na Zulfa Khatibu  mara alipofika katika wod ya akinamama
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumzana baadhi ya Wauguzi wa Hospitali hiyo
 Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Erwin Telemans akizungumza na waandishi wa habari
 Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Temeke, Amaani Malima akizungumza na waandishi wa habari
  Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Temeke, Amaani Malimaakisoma taarifa ya Hospitali hiyo
 Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Erwin Telemans akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi
   Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Erwin Telemans akimkabidhi zawadi mgeni rami

 Waziri Ummy akizungumza wakati wa hafla kukabidhi vifaa Tiba vya Afya ya Uzazi vilivyo fadhiliwa na CCBRT na kutembelea Wod za akinamama na Wodi ya watoto wa Kangaruu
 Sehemu ya madaktari na wauguzi


 Waziri wa Ummy katika picha ya pamoja na wafanyakazi mbalimbali wakiwemo madaktari
Waziri, Ummy katika picha ya pamja na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke. (PCHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages