Breaking News

Your Ad Spot

Jul 22, 2017

DK. KIGWANGALLA AFANYA ZIARA MIKOA YA RUKWA, KATAVI NA TABORA

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla ameendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua huduma za Afya ‘Imarisha Afya’ katika Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali mbalimbali kwenye mikoa ya Rukwa, Katavi pamoja na Tabora.  

Akiwa katika mkoa wa Rukwa, Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea Hospitali ya Sumbawanga ambayp ni ya Mkoa wa Rukwa na kujionea mambo mbalimbali huku akiwapongeza kwa namna walivyoboresha huduma zao ikiwemo ile ya Maabara, Chumba cha upasuaji na huduma zingine ambapo aliwaagiza kuhakikisha wanakuwa na hakiba ya kutosha ya damu salama kwa ajili ya dharura kwa wagonjwa wa ukanda huo. 

 Mbali na Hospitali ya Mkoa wa Rukwa, pia aliweza kutembelea kituo ca Laela ambapo pia mbali ya kujionea utendaji kazi wa kituo hicho alipongeza juhudi za Mbunge wa jimbo la Kwera, Mh. Ignas Alloyce Malocha kwa kushirikiana na wananchi wake katika masuala ya huduma za Afya.


 Ziara hiyo katika mkoa wa Rukwa, aliweza kumalizia katika Kituo cha Afya Wampembe kilichopo Wilayani Nkasi ambapo alijionea shughuli mbalimbali ikiwemo huduma za Upasuaji hata hivyo aliutaka uongozi wa kituo hicho ambacho kipo mwambao wa Ziwa Tanganyika kuhakikisha wanakamilisha mifum ya maji safi na salama ndani ya kituo pamoja na kuboresha huduma za Maabara na usafi kwa ajumla.  

Akiwa katika Mkoa wa Katavi, Dk. Kigwangalla aliweza kufanya ziara ya kushtukiza kituo cha Afya Inyonga,kilichopo Mlele majira ya Saa Sita mchana na kuweza kukagua maeneo mbalimbali ikiwemo Chumba cha Maabara, Chumba cha Upasuaji na wodi ya akina mama wanaosubiria kujifungua.  

Hata hivyo, Dk. Kigwangalla amemtaka Kaimu Mganga Mkuu wa Kituo hicho kumuandikia maelezo juu ya kutokuwepo kwa watoa huduma kwenye jingo la chumba cha upasuaji na eneo la wodi ya akina mama wanaosubiria kujifungua kwani licha ya kufika hapo hakukuta mtoa huduma hata mmoja kwa wakati huo hali ambayo inaweza kuleta hatari.  

“Nataka kupata maelezo kwa maandishi. Kwa nini hakukua na watoa huduma ndani ya Chumba cha upasuaji na kule kwa wodi ya wamama wajawazito. Nilifika kuwakagua kwa upande wa Maabara nimekuta safi mumeweza kuboresha huduma na mumezingatia maelezo yangu niliyoyatoa kipindi nilichofika kukagua mwaka jana. Lakini pia hali niliyoikuta katika maeneo hayo niliyotembelea bila kuwakuta wahusika hii ni hatari nitahitaji maelezo ya kimaandishi” alieleza Dk. Kigwangalla wakati akitoa maagizo kwa Kaimu Mganga Mkuu wa kituo hicho. 

 Aidha, akiwa katika mkoa wa Tabora, aliweza kutembelea eneo la jengo linalojengwa Hospitali ya Wilaya ya Uyui na baadae aliweza kumalizia ziara yake katika Zahanati ya Isikizya ambapo aliagiza Mkurugenzi wa Wilaya ya Uyui kuhakikisha wanatenga bajeti pamoja na kushirikiana na nguvu za wananchi na mbunge wa jimbo hilo wanajenga majengo ya kulazwa wagonjwa, chumba cha upasuaji, maabara na miundombinu mingine ili Zahanati hiyo ije kupanda na kuwa Kituo cha Afya kwani kinahudumia eneo kubwa katika mji huo wa Isikizya ambayo hipo ndani ya Makao makuu ya Wilaya hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikaguachumba cha upasuaji Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua Maabara ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikaguachumba cha upasuaji Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa viongozi wa Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akiingia chumba cha Wodi ya wanawake kituo cha Afya Laela Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akielekea kukagua Maabara ya Kituo cha Afya Laela Mkoa wa Rukwa
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Saidi Mtanda akihutubia wakati Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla alipotembelea kituo cha Afya Wampembe Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua kitanda ndani ya chumba cha kujifungulia katika kituo cha Afya Wampembe Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akitembelea kituo cha Afya Wampembe, Mkoa wa Rukwa. kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mh. Said Mtanda
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua mfumo wa maji unaoingia kituo cha Afya Wampembe, kutokea Ziwa Tanganyika, Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua chumba cha upasuaji mdogo cha Kituo cha Afya Nkasi alipotembelea hapo majira ya saa mbili usiku, Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua eneo litakalojengwa majengo ya utanuzi wa kituo hicho cha Afya ambapo kikikamilika kinatarajia kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akipatiwa maelezo ya maendeleo ya jengo linalojengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Uyui, Mkoani Tabora, kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini Mh. Almasi Maige
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua jengo litakalojengwa Hospitali ya Wilaya ya Uyui, Mkoani Tabora.
Jengo linaloendelea kujengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Uyui
 
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua ndani ya Maabara ya Kituo cha Afya Inyonga, Mlele, Mkoani Katavi
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akisaini kitabu cha wageni Kituo cha Afya Inyonga, Mlele, Mkoani Katavi

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages