Breaking News

Your Ad Spot

Jul 3, 2017

MWANANCHI MWANZA APATA NGEKEWA YA KUMUUZIA KARANGA MTAANI RAIS DK. MAGUFULI, LEO


Rais Dk. John Magufuli akifurahi wakati ameshika mfuko wake wa karanga alizonunua kwa mwanadada mmoja anayefanya biashara ya kuuza kwa kutembeza mitaani karanga hizo katikati ya jiji la Mwanza. Rais amewasili leo mjini Mwanza kuanza ziara ya siku mbili.
 "Hizi nadhani zinatosha", inaelekea ndivyo alivyokuwa akisema, Rais Dk John Magufuli baada kununua karanga kwa mwanadada mmoja anayefanya biashara ya kuuza kwa kutembeza mitaani karanga hizo katikati ya jiji la Mwanza. Rais amewasili leo mjini Mwanza kuanza ziara ya siku mbili
 Rais Dk. John Magufuli akiwasalimia wananchi katikati ya jiji la Mwanza waliokusanyika kumpokea, leo
 Rais Dk. John Magufuli akiwasalimia wananchi katikati ya jiji la Mwanza waliokusanyika kumpokea, leo

 Rais Dk. John Magufuli akiwasalimia wananchi katikati ya jiji la Mwanza waliokusanyika kumpokea, leo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mpira pamoja na Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela katika uwanja wa Nyamagana ambapo timu ya Buhongwa United ilikuwa ikicheza na Nyamwaga FC.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Wachezaji wa Buhongwa Fc mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Nyamagana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono washabiki wa mpira wa miguu wakati akitoka katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. PICHA NA IKULU
ALIPOWASILI 
 Rais Dk. John Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela  baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza, leo
 Rais Dk. John Magufuli akisalimiana na Viongozi wa Dini baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza
Rais Dk. John Magufuli akiangalia ngoma za asili kutoka kikundi cha Bujora mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza.PICHA: IKULU

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages