Breaking News

Your Ad Spot

Jul 6, 2017

RAIS ARIDHIA JAJI PROFESA RUHANGISA KUSTAAFU MAPEMA

IKULU, DAR ES SALAAM.
Rais Dk. John Magufuli ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Prof. John Eudes Ruhangisa.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, imesema, taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Rais Magufuli ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa Prof. John Eudes Ruhangisa kuanzia leo 06 Julai, 2017.  Prof. John Eudes Ruhangisa alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya  Tanzania kanda ya Shinyanga.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages