Breaking News

Your Ad Spot

Jul 15, 2017

RC SHINYANGA ATEMBELEA KIWANDA CHA MAFUTA YA MCHELE KIZUMBI SHINYANGA

Ijumaa Julai 15,2017,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack ametembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya mchele kinachomilikiwa na kampuni ya Mwekezaji kutoka nchi ya China Jielong Holding kilichopo katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.


Mkuu huyo wa mkoa aliyekuwa ameambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga na maafisa mbalimbali mkoa huo amejionea jinsi kampuni hiyo ilivyodhamiria kuzalisha mafuta ya kupikia yanatokana na mapumba laini ya mpunga “Mchele”.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Telack alisema kiwanda hicho ni cha pekee nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla na kitasaidia wamiliki wa mashine za kukobolea mpunga pamoja na wakulima kunufaika na zao la mpunga kwani wataweza kuuza mapumba kwa ajili ya kutumika kama malighafi kuzalishia mafuta hayo.

“Niwapongeze wawekezaji hawa kwa ubunifu huu wa kiwanda cha aina yake, serikali ya mkoa wa Shinyanga inaunga mkono jitihada za kuhakikisha tunakuwa na uchumi wa viwanda,tushirikiana kuwahamasisha wananchi kulima mpunga kwa wingi na wale wenye mpunga basi wauze mapumba yao ili wajipatie kipato”,alieleza Telack.

“Naamini watu wenye mashine za kukobolea mpunga wataongeza kipato kwa kuuza mabaki ya mpunga kwa ajili ya kuendeshea kiwanda hiki ambacho pia kinazalisha nishati ya umeme kwa kutumia mapumba”,alieleza Telack.

Aidha aliwahamasisha wamiliki wa kampuni ya Jielong Holding kununua mapumba ya mchele kwani katika maeneo mbalimbali mkoani Shinyanga ili kiwanda hicho kianze kufanya kazi mara moja.

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei aliiomba serikali kuendelea kushirikiana na kampuni hiyo na pale panapojitokeza mapungufu basi serikali iwape ushauri kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.

“Tunaishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa viwanda,lengo kampuni yetu inayojihusiha na mazao hususani uzalishaji wa mafuta ya alizeti,pamba na mchele na kutengeneza sabuni ni kuwainua kiuchumi wananchi kupitia mazao wanayolima”,alisema Shuwei.

Hata hivyo alisema kiwanda hicho kimekwama kuanza uzalishaji wa mafuta ya mchele kutokana na uhaba wa malighafi kwani zinatakiwa tani 500 za mapumba kwa ajili ya kuanzisha uzalishaji lakini kiwango hicho hakijafika.
Habari Katika Picha
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack (kulia) akitembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya mchele kinachomilikiwa na kampuni ya Mwekezaji kutoka nchi ya China Jielong Holding kilichopo katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.Kulia kwake ni Mkalimani katika kampuni hiyo Joseph Warioba akifuatiwa na Mwenyekiti wa kampuni Jielong Holding,Qi Qi Shuwei.Wengine ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga na maafisa kutoka mkoa huo.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwa ndani ya kiwanda cha Jielong Holding.
Qi Shuwei akiongoza msafara wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kuangalia uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na mazao yanayolimwa na wakulima.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiteta jambo na Mwenyekiti wa kampuni Jielong Holding,Qi Qi Shuwei.
Kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei akimweleza mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack kuhusu kiwanda cha mafuta ya mchele walichokianzisha ambapo watakuwa wananunua mapumba ya mpunga ili kupata mafuta ya kupikia.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei akionesha mapumba malaini yaliyoanza kutengenezwa ili kupata mafuta ya kupikia.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akishika mapumba laini ya mpunga 'mchele' ambayo tayari yapo katika hatua za awali kwa ajili ya kutengeza mafuta ya kupikia.
Mapumba ya mpunga yakiwa kiwandani.
Mkuu wa mkoa,waandishi wa habari na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga wakiangalia moto mkali ndani ya kiwanda hicho unaotokana na mapumba/mabaki ya nafaka ambayo yanatumika kutengeneza nishati ya umeme katika kiwanda cha Jielong Holding.Kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei.
Dirisha dogo lililofunguliwa kuonesha moto mkali.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei akimweleza jambo mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack wakati akimbelea viwanda vya kampuni hiyo.
Mkalimani katika kiwanda cha Jielong Holding,Joseph Warioba akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack kuhusu malighafi mbalimbali zinazotumika katika kiwanda hicho cha kutengeneza mafuta ya alizeti,pamba,mchele na sabuni.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia zoezi la utengenezaji wa madumu ya plastiki kwa ajili ya kuwekea mafuta yanayotengenezwa katika kiwanda cha Jielong Holding.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia mitambo ya kutengenezea vifungashio vya plastiki/madumu ya mafuta.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwa ndani ya kiwanda cha Jielong Holding.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia ndoo ya plastiki iliyotengenezwa katika kiwanda hicho kwa ajili ya kuwekea mafuta ya alizeti.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akingalia shughuli ya uzalishaji mafuta ya alizeti inavyofanyika.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia mafuta ambayo yako tayari kwa ajili matumizi ya binadamu.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwa ndani ya kiwanda hicho.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei akimweleza jambo mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia mitambo ndani ya kiwanda.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiendelea kuangalia mitambo.
Mfanyakazi wa kiwanda cha Jielong Holding,Joseph Warioba akionesha mitambo ya kutengenezea mafuta mbalimbali.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia sabuni ya gwanji iliyotengenezwa katika kiwanda cha sabuni cha Jielong Holding.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia sabuni.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack na Afisa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga Anna Maria Yondani wakiangalia miche ya sabuni.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akikagua mazingira nje ya viwanda
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiangalia shimo la majitaka.
Kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Jielong Holding, Qi Shuwei akizungumza baada ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack kutembelea viwanda vinavyomilikiwa na kampuni ya Jielong Holding.Kushoto ni Mkalimani wa kampuni hiyo Joseph Warioba akitafsiri lugha ya Kichina na Kiswahili.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza baada ya kutembelea viwanda,
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa,maafisa mkoa na wafanyakazi wa kampuni ya Jielong Holding wakijadiliana namna ya kufanya ili viwanda viwanufaishe wananchi,wawekezaji na serikali.
Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages