Breaking News

Your Ad Spot

Aug 15, 2017

ANNA ABDALLAH AWAPONGEZA GIRL GUIDES KWA KUIWAKILISHA VIZURI TANZANIA NJE YA NCHI

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha  Tanzania Girl Guides (TGGA), Anna Abdallah (katikati) akiwa na Girl Guides waliorejea nchini kutoka kwenye programu ya Yess ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya uongozi, utamaduni na maadili  katika nchi za Uganda, Madagascar,  Zimbabwe na Zambia. Hapo ilikuwa wakati wa hafla maalumu iliyoandaliwa na TGGA  Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapongeza na kupata mrejesho wa walichojifunza walipokuwa kwenye programu hiyo inayodhaminiwa na Norwey.Anna Abdallah aliwapongeza wasichana hao wanne kwa kuiwakilisha vizuri TGGA  na Tanzania katika programu hiyo nje ya nchi.

Kutoka kulia ni Ummy Mwabondo alikwenda Zambia, Farida Mjoge aliyekuwa Uganda,  Elizabeth Betha (Madagascar) na Edna Chembele (Zimbabwe),


 Girl Guides hao wakipata msosi wakati wahafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa kwa ajili yao kwenye Hoteli ya Golden Tulip, Oysterbay, Dar es Salaam.
 Anna Abdallah akiotoa nasaha na pongezi kwa Girl Guides kwa kuiwakilisha vizuri TGGA NA Tganzania kwa ujumla, ambapo aliwataka watumie mafunzo waliyoyapata kwa kutoa mafunzo kwa wasichana wenzao nchini.
 Wakiwa na furahani Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi (kushoto), Anna Abdallah (katikati) na Mjumbe wa TGGA, Agnes Makenya
 Katibu Mkuu wa TGGA Tanzania, Grace Shaba akitoa neno la ukaribisho muda mfupi kabla ya Girl Guides waliorejea nchini kutoka nje ya nchi kwenye programu hiyo kuelezea mambo mbalimbali waliyoyafanya na kujifunza
 Grace Shaba akiwatambulisha Girl Guides hao
 i Ummy Mwabondo akielezea kwa njia ya picha kazi mbalimbali alizokuwa anazifanya alipokuwa Zambia
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, ambaye ni Mjumbe wa  Bodi ya TGGA, Sophia Mjema akitoa ufafanuzi wakati Girl Guides wakielezea mafanikio na changamoto ya mafunzo yao nje ya nchi
 Girl Guides Farida akielezea mambo mbalimbali aliyoyafanya akiwa Uganda kwa muda wa miezi sita.
 Viongozi na wageni waalikwa wakionesha ishara ya TGGA
 Viongozi wa Girl Guides Makao Makuu ya TGGA wakiwa na furaha wakati wa hafla hiyo
 Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi (kushoto), akiwa na Kamishna wa Kimataifa wa TGGA wakijadili jambo
 Sasa ni wakati wa msosi
















 Mwenyekiti wa TGGA, Profesa Martha Qorro akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya TGGA, Anna Abdala kuzungumza katika hafla hiyo.
 Mwakilishi wa wazazi wa Girl Guides hao, Florence Gondwe akitoa shukrani kwa TGGA kwa kuwapatia wasichana hao fursa ya kwenda nje ya nchi kwenye programu hiyo ambayo alidai itawasaidia sana kimaisha.
 Kamishna Hangi akitoa neno la shukrani kwa viongozi waliohudhuria hafla hiyo pamoja na Girl Guides
 Wakiwa katika picha ya pamoja


Anna Abdallah akiagana na Girl Guides baada ya hafla kumalizika

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages