Breaking News

Your Ad Spot

Aug 25, 2017

RAIS DK.SHEIN AFANYA ZIARA WILAYA YA CHAKE CHAKE PEMBA

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akisalimiana na Viongozi mara alipowasili katika Kijiji cha Kiziwani Shungi Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba leo akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya hiyo.( Picha na Ikulu)
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipofika kutembelea Shamba la Mikarafuu na kuendelea na zoezi la uchumaji wa Karafuu katika Kijiji cha Kiziwani Shungi Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya hiyo leo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akimsalimia Mtoto Samira Mussa miezi Miwili aliyechukuliwa na dada yake Lussia Mussa Miaka Kumi na tano wanaoishi katika Kijiji cha Kiziwani Shungi Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba,aliwasalimia baada ya   kutembelea Shamba la Mikarafuu leo,akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya hiyo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akisalimiana na Viongozi mara alipowasili katika Kijiji cha Kiziwani Shungi Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba leo akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya hiyo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kulifungua Tawi la CCM Tibirinzi leo akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba kutembelea na kukagua Miradi mbali mbali ya Maendeleo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akikata utepe kufungua  Tawi la CCM Tibirinzi leo akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba kutembelea na kukagua Miradi mbali mbali ya Maendeleo,(kushoto) Mwakilishi wa Jimbo la Chakechake CCM Mhe. Suleiman Sarakhani Said.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akikagua Tawi la CCM Tibirinzi leo baada ya kulifungua akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba kutembelea na kukagua Miradi mbali mbali ya Maendeleo,(kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdalla Juma Abdalla (Mabodi). 
Baadhi ya Wanachma wa Chama cha Mapinduzi CCM wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na Wanachama hao Tawi la CCM Tibirinzi leo baada ya kulifungua rasmi akiwa katika mwendelezo wa ziara yake katika Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba kwa kutembelea na kukagua Miradi mbali mbali ya Maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages