Breaking News

Your Ad Spot

Oct 19, 2017

AMUUA MWENZAKE KWA ULEVI CHALINZE MKOA WA PWANI

Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
Mfugaji Lemandra Kishakwi (35) mkazi wa Chamakweza, Chalinze mkoani Pwani, ameuawa kwa kuchomwa kisu maeneo mbalimbali ya mwili na mwenzake Niniyay Silongoy chanzo kikidaiwa ni ulevi.

Aidha jeshi la polisi mkoani hapo, limekamata bangi gunia saba zikiwa kwenye mifuko ya salfet ambazo zina uzito wa kg 7,500 .

Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ,(ACP)Jonathan Shanna akielezea tukio la mauaji alisema limetokea octoba 18 majira ya saa 11.30 jioni,huko Chamakweza.

Alisema kuwa ,Lemandra ambae ni (mmasai )mfugaji aliuawa kwa kuchomwa kisu maeneo ya kwapa la kushoto ,shingoni na mkono wa kulia wakati wakiwa kwenye ulevi.

Kamanda Shanna ,alielezea mtuhumiwa alikimbia kusikojulikana baada ya kufanya tukio hilo na polisi inaendelea na juhudi za kumtafuta .

Mwili wa marehemu umekabidhiwa kwa ndugu wa marehemu mara baada ya uchunguzi wa daktari kukamilika.

Akielezea kuhusiana na tukio la kukamata bangi ,kamanda Shanna alisema askari wakiwa doria eneo la Kwamatias Kibaha ,walipata taarifa kuwa kuna ajali ya gari no.T847 DHT aina ya I.S.T.

"Walipofika eneo la tukio waliwaokoa majeruhi Gudluck Kundaeli Mbowe (24)mkazi wa Kiwalani jijini Dar es salaam aliyekuwa dereva wa gari hilo na Ally Mtena (28) mkazi wa Gongolamboto "

"Wakati wanapekua gari hilo waliikuta ikiwa na gunia saba za bangi zikiwa kwenye salfet ,zenye uzito wa kg 7,500.:";

Kamanda huyo wa polisi mkoani humo ,alibainisha watuhumiwa wamekamatwa ili kuweza kuchukuliwa hatua za kisheria .

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages