Breaking News

Your Ad Spot

Oct 20, 2017

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KIONGOZI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA URUSI NA KIONGOZI WA BUNGE LA NCHI HIYO

 Spika wa Bunge, Job Ndugai (kushoto) akivishwa nishani maalum ya maadhimisho ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi na Kiongozi wa Chama cha kikomunisti cha Urusi, Komredi Gennady Zyuganov ambae ni Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo, Spika alipotembea leo ofisini kwa kionhozi huyo akiwa Urusi ambako anashiriki Mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani.
 Spika wa Bunge Job Ndugai (kushoto) akimkabidhi zawadi Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo Komredi Gennady Zyuganov, alipomtembelea ofisini kwa kiongozi huyo. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini humo, Jenerali Mstaafu Wynjones kisamba. Spika Ndugai yupo nchini Urusi kushiriki mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani
Spika wa Bunge, Job Ndugai (wa pili kulia)akifanya mazungumzo na Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo, Komredi Gennady Zyuganov (wa pili kushoto) alipomtembelea leo ofisini kwa kiongozi huyo katika maadhimisho ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi. Spika Ndugai yupo nchini Urusi, akishiriki Mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani unaoendelea Jijini St. Petersburg, Urusi

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages