Baraza la Mabalozi wa
Kiarabu nchini Tanzania linathamini upigaji kura wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kupitisha rasimu ya azimio linalohusu Mji wa Jerusalem,
lililopitishwa Alhamisi ya tarehe 21 Desemba 2017, katika utaratibu
wa Kikao cha Kumi Maalumu cha Dharura cha Mkutano Mkuu wa Umoja wa
Mataifa, chini ya kichwa cha habari kisemacho “Matendo ya Israeli yasiyo
ya kisheria Jerusalem ya Mashariki inayokaliwa kimabavu na maeneo
mengine ya Palestina yanayokaliwa kimabavu”, azimio lililopitishwa baada
ya nchi 128 kulipigia kura ya ndio, huku nchi 9 zikilipinga ikiwemo
Marekani na Israeli.
Kwa mnasaba huu, Baraza na Mabalozi wa Kiarabu linatilia mkazo kuthamini kwake msimamo huu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, nao ni msimamo unaoonesha hali ya kwenda sambamba na misingi muhimu iliyowekwa na Kiongozi Muasisi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, katika yale yahusuyo kuheshimu uhalali wa kimataifa na haki za mataifa katika kujipangia mustakabali wake na kukabiliana na ukoloni na uvamizi wa kigeni.
Kwa mnasaba huu, Baraza na Mabalozi wa Kiarabu linatilia mkazo kuthamini kwake msimamo huu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, nao ni msimamo unaoonesha hali ya kwenda sambamba na misingi muhimu iliyowekwa na Kiongozi Muasisi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, katika yale yahusuyo kuheshimu uhalali wa kimataifa na haki za mataifa katika kujipangia mustakabali wake na kukabiliana na ukoloni na uvamizi wa kigeni.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269