Breaking News

Your Ad Spot

Aug 23, 2010

KAMPUNI MPYA YA SIMU ZA MKONONI YA HITS YAZINDUA NEMBO YAKE

Hits Tanzania kuzinduliwa Januari 2011

Kampuni ya ExcellentCom inayoendesha shughuli zake kama Hits Tanzania imefanya uzinduzi wa chapa na nembo yake ya “hits” siku ya Jumatatu, tarehe 23 August 2010 kwenye hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam. Hits Tanzania ni kampuni inayoendesha mtandao wa mawasiliano ya simu ambayo imepewa leseni ya kutoa huduma za Sauti, ujumbe mfupi na huduma za Mtandao (Data).

Wakati wa uzinduzi wa nembo yake, mwenyekiti wa Excellentcom Tanzania Ltd, Mhe. Abdullah Mwinyi alisema “Hits Tanzania sasa imeanza rasmi shughuli zake na iko kwenye hatua za mwisho kuwasha mitambo yake, kwa hiyo tutaanza ujenzi na upanuzi wa mtandao ili kuwa na uwezo wa kutoa huduma zetu nchi nzima mapema mwakani".

Akizungumza na waandishi wa habari, Afisa Mtendaji Mkuu wa ExcellentCom, David Charles alisema kwamba kwa mujibu wa taarifa ya TCRA (Tanzania Communications Regulatory Authority) ya Machi 2010, soko la huduma za simu za mkononi kwa sasa zinapatikana kwa kuwafikia zaidi ya asilimia 40 ya wananchi wa Tanzania. Aliongeza kwamba na kwa mujibu wa taarifa ya BMI (British Market Index) ya awamu ya pili ya mwaka 2010, matarajio ni kwamba huduma hizo zitawafikia zaidi ya asilimia 60 ya wananchi ifikapo 2012.

Bw. Charles alisema kwamba tayari kuna uwekezaji endelevu wa miundombinu kadhaa ya mawasiliano ambayo inashawishi kuwapo kwa mikakati ya ubia endelevu. “Kusema kweli, imeonekana dhahiri kwamba hakuna wakati muafaka kwa kampuni ya Hits Tanzania kusambaza mtandao wake kama sasa,” alisema.

Kampuni itaendelea na harakati za kuwekeana mikataba na wabia muhimu ambao wataiwezesha kampuni hiyo kuwapa wateja wa Hits na wateja wa wabia huduma maalum hapo ifikapo mwakani. Kwa mtazamo huo, kampeni hiyo itaitwa "a life time subscription" ambayo itatoa thamani na ubora kwa wabia wa Hits pamoja na wateja wake.

Hits Tanzania itazindua kampeni ya kutenga namba ya simu baadae mwaka huu, ambapo wateja wataweza kutengewa namba zao kupitia kianzishi namba cha Hits, ambacho ni 0741 mpaka 8.

English vesion

Hits Tanzania to launch in January 2011

Dar Es Salaam, August 23rd, 2010:

ExcellentCom trading as Hits Tanzania revealed its brand and logo “hits” to the public on Monday the 23rd August 2010 at the Movenpick Hotel. Hits Tanzania is a telecommunication network operator with a license to offer Voice, SMS and Data Services.

During the unveiling of the brand, the Chairman of Excellentcom Tanzania Ltd, Hons. Abdullah Mwinyi said that “Hits Tanzania operation is now in the final stages to go live and we will roll out a nationwide coverage by early next year.

Speaking to the media, ExcellentCom CEO David Charles said that according to TCRA (Tanzania Communications Regulatory Authority) 2010 March report, the cellular market in Tanzania currently has a penetration of over 40%. And according to BMI (British Market Index Q2 report, 2010) the projection is expected to reach over 60% in 2012.

He added that there are a number of network infrastructures in place that encourage synergies and strategic partnership. “Clearly there is never been a better time for Hits Tanzania to rollout its’ network than now,” He said.

The company will embark in signing partnership deals with a number of potential partners that will see them offer their customers and Hits customers with bundling packages comes next year. The campaign will be called “a life time subscription” that will create value to Hits partners and its customers.

Hits Tanzania will launch the reserve a number campaign later this year, where customers will be able to reserve their numbers on the Hits prefix which will be the 0741- 8.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages