Thursday, February 02, 2012

CCM YAUKABIDHI MKOA WA MARA TANI ZA SARUJI KWA AJILI YA UJENZI WA MADARASA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akimkabidhi mifuko  ya saruji  mkuu wa mkoa wa Mara  John Tupa, katika hafla iliyofanyika leo Ofisi ya mkuu huyo wa mkoa. Saruji hiyo ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari mkoani humo kuwezesha wanafunzi waliofaulu mwaka huu kupata  madarasa ya kutumia. Kulia ni makada wa CCM waliotoa saruji hiyo. Zulfikar Nanji wa Kampuni ya Mwanza Huduma Ltd (mifuko 400) Joseph 'Msukuma' Kasheku mfanyabiashara ambaye pia Diwani wa Kata ya Nzela, Geita na Mjumbe wa NEC, Vedastus Mathayo ambao wote wametoa mifuko 100 kila mmoja.

HABARI KAMILI

NA BASHIR NKOROMO, MUSOMA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeukabidhi mkoa wa Mara tani za saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mkoani humo ikiwa ni sehemu ya maadhimnisho ya miaka 35 ya CCM.

Saruji hiyo itatumika kujenga madarasa kwa ajili ya wanafunzi ambao wameshindwa kuanza kidato cha kwanza kutokana na uhaba wa madarasa licha ya kufaulu mwaka huu.

Akikabidhi mifuko hiyo kwa mkuu wa mkoa huo, John Tupa, Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema saruji hiyo imetolewa na makada wa CCM ambao wameamua kutoa mchango huo kwa kupitia CCM ikiwa ni kuunga mkono maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM.

Nape alisema makada hao ni Zulfikar Nanji wa Kampuni ya  Mwanza Huduma Ltd (mifuko 400) Joseph 'Msukuma' Kasheku  mfanyabiashara ambaye pia Diwani wa Kata ya Nzela, Geita na Mjumbe wa NEC, Vedastus Mathayo ambao wote wametoa mifuko 100 kila mmoja.

Alisema kada mwingine ni Dk. Isack Chacha Ng'ariba ambaye aliahidi kutoa tani 200 za saruji ahadi ambayo aliitoa papo hapo wakati wa makabidhiano hayo.

Nape aliwashukuru wafanyabiashara makada hao wa CCM kwa kuiunga mkono CCM katika kuhakikisha kwamba sherehe za miaka 35 ya CCM inakuwa na mafanikio makubwa kwa kutekeleza azma ya kuchangia shughuli za maendeleo.

Alisema, wafanyabiashara na makada hao wanaichangia CCM pia kama kuonyesha shukurani yao kwa kuweza kufanya biashara zao kwa miaka mingi katika mazingira ya amani na utulivu chini ya uongozi wa serikali ya CCM.

"Mkiona vinaelea vimeundwa, amani na utulivu huu uliopo ni mazingira yaliyojngwa na kuendelea kutunzwa na CCM tangu ilipoanza kutawala nchi hii baada ya kurithi uongozi kutoka vyama vya TANU NA ASP miaka 35 iliyopita", alisema Nape.

Akipokea msaada huo, Mkuu wa mkoa alisema, jumla ya watoto  6486 kati ya asilimia 50.3 ya watoto waliofaulu, wameshindwa kuanza kidato cha kwanza mkoani mwake kutokana uhaba wa vyumba vya madarasa licha ya kufaulu.

Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa unahitaji madarasa 718 wakati yaliyopo ni 479 na hiyo kuwa na upungufu wa madawati 239 na kwamba wilaya ya Bunda ndiyo inayoongoza kuwa upungufu wa madarasa.

Alisema licha ya kupata msaada huo wa saruji bado mkoa unahitaji mabati, mbao na madawati kwa ajili ya madarasa yatakayojengwa.

Wednesday, February 01, 2012

LIBENEKE JIPYA LA 'Rural and Urban '

Heshima zenu Wadau wote Nilikuwa napenda Kuwatambulisha Kwenu Blog  mpya ya Rural and Urban ambayo  itakuwa ikizungumzia maisha hayo zaidi ya mjini na Vijijini. Karibuni sana ukiona Link hii mpatie na mwengine. Natanguliza Shukrani zangu asanteni. Kutembelea Libeneke hili Bofya 

Tuesday, January 31, 2012

VIJANA MWANZA WAJINOA KWA AJILI YA GWARIDE LA 'KUFA MTU' KWENYE SHEREHE ZA KILELE CHA MIAKA 35 YA CCM

Vijana wa CCM kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza , wakiwa katika siku ya pili ya mazoezi ya gwaride maalum la sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, sherehe hizo pia zitafanyika Kitaifa katika Uwanja huo ambapo mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete
 Vijana wa CCM wakionyesha ukakamavu wao wakati wa mazoezi hayo leo
 Vijana wa CCM wakifanya mazoezi jisni watakavyokuwa wakitoa saluti kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete wakati wa gwaride maalum watakalocheza siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, Jumapili ijayo, Februari 5, 2012
 Makamanda wa gwaride hilo nao wakifanya mazoezi kuhakikisha kwamba watakuwa hodari siku hiyo
 Kama kawaida hakuna gwaride bila brass band. Hawa vi vijana waliokuwa wakifanya mazoezi leo kwa ajili ya gwaride hilo la Februari 5, yaani Jumapili ijayo.
 Vikosi vya vijana hao vikiwa katika mazoezi ya kutembea katika gwaride leo
Kutokana na vijana hao kuweka kambi kwenye Uwanja huo ili kufanikisha maandaloizi yao hupata chakula na chai humo humo uwanjani. Hapa msosi unaandaliwa na vijana wenzao kwa ajili yao.

KATIBU WA NEC YA CCM, OGANAIZESHENI CCM ASHA ABDALLAH JUMA KATIKA MATIBABU INDIA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Oganaizesheni, Asha Abdallah Juma 'Mshua'  akiwa na wauguzi wa Hospitali ya MIOT nchini India baada ya kufanyiwa matibabu ya mguu kwenye hospitali hiyo, Kiongozi huyo wa CCM ambaye alienda nchini India mwishoni mwa mwaka jana hali yake inaendelea vizuri.
  Katibu wa NEC, Oganaizesheni CCM, Asha Abdallah Juma akiwa na  Profesa Mohandas, Mkuu wa Hospitali hiyo ya MIOT ( PICHA KWA HISANI YA  ASHA ABDALLA JUMA, INDIA).

SAMWEL DANIEL NA KAINDI TARATIBU WAMEREMETA

Wakiwa na nyuso za furaha bwana harusi Samwel  Daniel  na mkewak e Kaindi  Taratibu wakiw a kwenye pozi la  picha baada ya kufunga ndoa yao katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kibaha hivi karibuni na kufuiatiwa na sherehe kubwa iliyofanyika katika ukumbio wa Mbezi   Luxiry jijini Dar es Salaam.
 Bwana Harusi Samwel  Daniel  na mkewak e Kaindi  Taratibu wakiwa katika pozi la upendo 
Samwel  Daniel  na mkewak e Kaindi  Taratibu wakipozi mbele ya gari lao la harusi la kifahari
.  Bibi harusi akipita juu ya migongo ya wakwe zake wakati wa kuingia ukumbini ikiwa ni ishara ya kukaribishwa katika familia, kabila la Wayao .
Bwana harusi akipita juu ya migongo ya wazazi wake wakati wa kuingia ukumbini wakati wa harusi yake iliyofanyika katika ukumbi wa Mbezi Luxiry jijini ,Dar es Salaam.utamaduni huu hufanywa na watu wa lindi kabaila la wayao. 
Makaka wa bwana harusi wakiwa katika picha ya pamoja wakisherehekea harusi ya mdogo wao .
Siwa wili tena ni mwili mmoja ,bwana harusi  Samwel akiwa na mkewa Kaindi wakishuka kutoka katika mlima kilimanjaro  uliopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam, walipokwenda kufanya utalii wa ndani.baada  ya kufunga ndoa yao kwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Januari 28. (picha zote na Albert)