Breaking News

Your Ad Spot

Nov 29, 2010

PROFESA ANNA TIBAIJUKA AKABIDHIWA OFISI NA CHILIGATI

Aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mh. John Zefania Chiligati (kushoto) akimkabidhi nyaraka mbalimbali za kutendea kazi Waziri mwenye dhamana hiyo Mh. Prof. Anna Tibaijuka. Makabidhiano hayo yalifanyika mara baada ya Mh. Tibaijuka kuingia ofisini jana tangu aapishwe. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara Mh. Patrick Rutabanzibwa. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Anna Tibaijuka, (wa Pili kutoka kulia, waliokaai) akiwa pamoja na Waziri aliyemaliza muda wake Mh. John Chiligati (kulia kwake), wakurugenzi na wakuu wa Vitengo, baada ya makabidhiano ya ofisi. Wengine (waliokaa) ni Naibu Waziri wa Wizara Hiyo Mh. Goodluck Ole Medeye (kulia kwa Mh. Chiligati), Katibu Mkuu Bw. Patrick Rutabanzibwa (wa kwanza kulia) na Naibu Katibu Mkuu Bibi Maria Bilia ( wa kwanza kushoto)

1 comment:

  1. Viwanja vya wazi vinauzwa sana, kazi kwako mama. Katibu Mkuu mchapakazi unae

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages