Breaking News

Your Ad Spot

Mar 28, 2011

TUWAENZI WAHANGA WA BIASHARA YA UTUMWA-BAN KI MOON

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, kushoto wake ni Naibu wake, Dkt. Asha-Rose Migiro na kulia  Bw. Joseph Deiss, Rais wa Baraza Kuu la 65 la Umoja wa Mataifa, wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kuwakumbuka wahanga wa utumwa na biashara ya utumwa, maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila  March 25 yalifanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Na Mwandishi Maalum
Mwishoni mwa wiki, Umoja wa Mataifa uliadhimisha siku ya Kimataifa ya kuwakumbuka wahanga wa utumwa na biashara ya  utumwa.
Maadhimisho  hayo ambayo ujumbe wake kwa  mwaka huu ulikuwa “ the  living legacy of 30 million untold stories” hufanyika kila  March 25 yaliambatana na  makongamano, maonesho ya dhana zilizotumika kusafirishia watumwa, ngoma za kiafrika  na  vyakula vya asili ya afrika.
Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban Ki Moon,  pamoja na mambo mengine amesisitiza haja na umuhimu wa kuendelea kufundishwa kwa  historia ya utumwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Ban Ki Moon  anasema kwa kufundisha na kujifunza historia ya utumwa na biashara ya utumwa pamoja na  madhara makubwa yaliyotokana na  biashara hiyo,  itakuwa ni njia moja wapo ya kuwaenzi wahanga wa utumwa. Lakini pia kujifunza nini kilipelekea kuanzishwa kwa biashara hiyo.
Akasema kuwa  UNESCO imefanya kazi kubwa ya  kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu na matukio ya kutisha  na  utumwa na biashara ya utumwa. Lakini anakiri kuwa bado kuna mengi ya kujifuza  kuhusu mamilioni ya waafrika walioathirika na biashara hiyo. kwamba kazi hiyo inatakiwa kuendelea mashuleni na katika maeneo mengine.
Katibu Mkuu wa UM, katika mazungumzo yake, amesisitiza kuwa biashara hiyo ya utumwa ilikuwa ni moja ya biashara mbaya sana iliyokandamiza na kuudhalilisha utu na hadhi ya mtu mweusi na kwamba  madonda   biashara hiyo bado yapo hadi leo hii.
“ kwa kuadhimisha siku hii ya kimataifa,  ni sehemu ya kuwakumbuka wahanga wa utumbwa,  tunatambua utu wao, heshima yao, kudhalilishwa kwao na mateso waliyoyapata” anasisitiza Ban Ki Moon
Na kuongeza kuwa maadhimisho haya pia yanalenga kutambua mchango wa wale wote waliojitolea  mhanga licha ya hatari kubwa iliyowakabilia kuipinga na hatimaye kumaliza biashara ya utumwa. 
 “ Hili hasa ndio kusudio la maadhimisho ya siku hii ya kimataifa ya watu wa asili ya afrika. Na ndio maana  mchakato wa ujenzi wa mnara wa kumbumbu ya biashara ya utumwa  unaendelea   kama njia moja wapo ya kuendelea kuwaenzi wahanga hao.” Anaeleza zaidi
Kwa Mujibu wa Katibu Mkuu,  maadhimisho hayo   pia yalikuwa yanalenga kutambua  mchango  na  juhudi za wanaharakati ambao hadi leo hii wanaendelea na kazi ya kupigania na  kupinga  aina mbalimbali za ukandamizaji na ukiukwaji wa haki za binadamu.
 Aidha  Ban ki Moona, anasema  kuwa ingawa  miaka 400 imepita tangu kukomeshwa kwa biashara ya utumwa, kumeibuka  aina mpya ya utumwa, anautaja utumwa huo kuwa ni ndoa za umri mdogo, usafirishaji haramu wa watoto, uuzwaji wa wanawake, na utumwa wa madeni unaowalazimu baadhi ya sehemu ya jamii kufanya kazi kwa muda mrefu kulipia madeni ya familia zao.
 “Ni vema tukautambua ukweli wa biadhara ya utumwa,   hebu basi  na tuwakumbuke wahanga  hao.  lakini lazima  pia tukumbuke na aina mpya  ya utumwa unaoendelea katika jamii zetu na  tukusanye nguvu za kuukabili  utumwa huu mpya” anasisitiza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages