Breaking News

Your Ad Spot

Sep 30, 2011

UCHAGUZI IGUNGA: VIJANA WAMCHANGAMKIA DK.KAFUMU, KINA MAMA NDIO USISEME

"KULA TANO" mgombea Ubunge Jimbo la Igunga kwa tiketi ya CCM, Dk. Dalaly Kafumu (kulia) akisema hivyo wakati akisalimiana na vijana wa Kata ya Usongo, akiwa katika mkutano wakampeni za CCM za uchaguzi mdogo jimboni humo. Katikati ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde ambaye alikuwa mkuu wa msafara wa kampeni hizo.
  Dk. Kafumu akiwasalimia wananfunzi wa shule ya msingi Usongo waliojumuika kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika leo katika kijiji hicho. 
Kina mama wakimlaki Dk. Kafumu aliposhuka kwenye helkopta kwenda kuwahutubia wananchi wa Mpogolo

Dk. Kafumu akivutwa huku na huko na mashabiki wake wakati akitaka kuondoka baada aya kampeni kata ya Ziba. Karibu yake ni mkuu wa msafara wake, mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde
Lusinde akimnadi Dk. Kafumu huku wananchi wakishangilia baada ya kufika kwa helkopta jioni, katika kijiji cha Lugubu Kata ya Itumba ambako ni kijijini kwa mgombea huyo
Watu wakimsikiliza kwa makini Dk. Dalaly wakati akihutubia mkutano wa Nsimbo. Unaweza kumuona mbwa huyu naye akiwa ametulia kwa amani kutokana na mkutwnao huo kuwa wa utulivu
Dk. Magufuli akimnadi kwa raha zote Dk. Kafumu katika mkutano uliofanyika Kata ya Ziba. Watatu kulia ni Mratibu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba
Dk Dalaly na Lusinde wakichana anga kwa helkopta kwenda kwenye mikutano ya kampeni leo
Mapolisi nao hawakuwa wakicheza mbali kuhakikisha usalama unakuwa timilifu kwenye mikutano yote ya kampeni
Igunga yenyewe ndiyo hii. katikati ni barabara ya Singida-Nzega kupitia Igunga

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages