Breaking News

Your Ad Spot

Dec 22, 2011

MAJAJI WATANZANIA WAPETA UCHAGUZI UMOJA WA MATAIFA

Jaji William Hussein Sekule (pichani) na Jaji Joseph Chiondo Masanche wote kutoka Tanzania  wameingia katika orodha ya majaji wa Mfumo mpya wa Kimataifa wa kushughulikia kesi za Mashauri ya Masalia ya Mahakama za Makosa ya Jinai ( International Residual  Mechanism for Criminal Tribunals) majaji hao wameingia katika orodha hiyo wakiwa ni kati  ya majaji 25 walioshinda baada ya kupingiwa kura ya siri miongoni mwa majaji 36 walioomba nafasi hiyo. Upigaji kura huo ulifanywa na Baraza Kuu la 66 la Umoja wa Mataifa na umekamilika siku ya Jumanne wiki hii.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages