Breaking News

Your Ad Spot

Jun 29, 2012

NAIBU KAMANDA VIKOSI VYA AMANI DARFUR AKUTANA NA NAAFISA UBALOZI WA TANZANIA UN

 Meja Jenerali  Wynjones Kisamba, Naibu Kamanda wa Vikosi  vya kulinda amani katika Jimbo la Darfur akibadilishana mawazo na baadhi ya maafisa wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, katika mazungumzo  yake na maafisa hao, Meja Jeneral amezungumza kwa kina fursa za uwekezaji zilizopo  katika nchi  ya Sudani ya Kusini namna gani Tanzania na watanzania  kama wakijipanga na wakithubutu watakavyoweza kunufaika na fursa hizo ambazo amesema kwa sasa zimechangamkiwa sana na majirani zetu ili hali Tanzania bado tukisuasua. Akazungumzia pia kuhusu operesheni ya kulinda amani huko darfur na changamoto zake, lakini pia  uwepo wa fursa ya Tanzania kupanua ushiriki  wake katika eneo hilo.
 Baadhi ya Maafisa wa Ubalozi wakiwa  katika picha ya pamoja na  Meja Jenerali Kisamba, ambapopia alitumia mazungumzo yake na maafisa hao  kuwashukuru na kwa kazi nzuri ya kuiwakilisha Tanzania katika Umoja wa Mataifa, huku akiwataka kuto legeza kamba katika kutetea maslahi ya nchi na vile vile kutoa ushauri endelevu katika masuala mbaliambali yanayohusika na utekelezaji wa majukumu yao.  HABARI KUHUSU TUKIO HILO BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages