Breaking News

Your Ad Spot

Nov 29, 2012

WATANZANIA WAISHIO UJERUMANI KUMUAGA BALOZI AHMADA NGERERA DESEMBA 8, MWAKA HUU MJINI BERLIN


Umoja wa Tanzania Ujerumani (UTU) unaheshima kubwa kutarifu na kuwaomba watanzania wote wanaoishi ujerumani na jirani ya Ujerumani kuwa umoja wetu tunatarajia kufanya afla ya kumuaga
Mheshimiwa balozi  Bw. Ahmada Ngemera ambaye anamaliza mda wake wa kufanya kazi,

Hafla hiyo itafanyika mjini Berlin siku ya Jumamosi tarehe 8.12.2012 .

Mhe.Balozi bwana Ahmada Ngemera  (pichani) amekua balozi wa Tanzania nchini Ujerumani na watanzania wanaoishi ujerumani watamkumbuka daima Mheshimiwa Balozi Bw.Ahmada Ngemera kwa kuwa karibu sana na jamii ya watanzania,pia atakumbukwa kwa jitihada zake au kile ambacho watanzania wa ujerumani wanachokiita kuasisi Umoja na mshikamano wa watanzania nchi ujerumani, ambapo Mhe.Balozi Bw.Ngemera na msaidizi wake Mhe.Bw.Ali Siwa wahamua kuhamasisha watanzania waishio Ujerumani kuungana katika kila hali kuanzisha umoja wa mshikamano wa watanzania,kitu ambacho mabalozi wengi walishindwa kufanikiwa kufanya labda kwa sababu ya ukubwa wa nchi ya ujerumani wa watanzania wanaishi katika miji mbali mbali,lakini kazi hiyo ya kuwaungunganisha watanzania, Balozi Bw.Ahmada Ngemera na Msaidizi wake Bw.Ali Siwa walifanikiwa kuwafikia
 watanzania wote waishio Ujerumani na kuwashauri waanzishe umoja wa mshikimano, na matunda ya juhudi zao ndipo kukazaliwa Umoja wa waTanzania Ujerumani.(UTU)  Umoja ambao ni chombo cha watanzania wote ! chombo ambacho watanzania waishio ujerumani wanajivunia !

UMOJA NA MSHIKAMANO NDIO MSINGI WETU IMARA!
OMBI:TUNAWAOMBA WATANZANIA WOTE ! NA MARAFIKI WOTE WA TANZANIA
AMBAO WANATAKA KUSHIRIKI KATIKA AFLA HII,TUNAOMBA MTOE MCHANGO WA EURO 20.00 NA KWA WANAFUNZI EURO 10.00 TU
 kwa kupitia Account : Union of Tanzania in German e.V.
VR Bank Rosenheim-Chiemsee AG
Konto-No.: 59641   BLZ: 71160161
Verwendungszweck: „Kumuaga Mhe. Balozi Ngemera

Pia unaweza kuwasiliana na kamati.utu@googlemail.com
simu namba +491734297997 au Katibu simu namba 01734744265 .

1 comment:

  1. I love your blog.. very nice colors & theme. Did you create this website yourself or did you hire someone to do
    it for you? Plz answer back as I'm looking to design my own blog and would like to find out where u got this from. kudos
    Also visit my webpage :: van nelle zware

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages