Breaking News

Your Ad Spot

Jan 29, 2013

KINANA ATINGA WILAYANI KAKONKO MKOANI KIGOMA, APOKEWA NA DIWANI WA CHADEMA KATA YA KASANDA

Kinana akipata maelezo  kwa Dc Kakonko, Peter Toima wakati akikagua mradi wa ujenzi nyumba za zahanati ya Kata ya Kasanda wilayani humo. Kulia ni diwani wa Kata hiyo Dickson Barutwa. 
Diwani wa kata ya Kasanda, Kakonko mkoani Kigoma, Dickson Barutwa (CHADEMA), akimpa malezo Kinana kuhusu ujenzi wa nyumba za zahanati ya kata hiyo unaofanywa na serikali
Kaimu Mganga Mkuu wa Kibondo,  Dk. Laurean Kanaganwa(kulia) akitoa maelezo ya zahanati ya kata ya Kasanda. Wapili kulia ni diwani wa Kasanda-Chadema, Dickson Barutwa 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na mabalozi wa mashina na wazee katika Kata ya Kasanda, Kakonko mkoa wa Kigoma
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi ya CCM mwanachama mpya, Elizabeth Gwimo, alipopokwa wanachama wapya 45, katika mkutano uliofanyika Kata ya Kasanda, Kakonko Kigoma
 Wanachama wapya wakila kiapo, baada ya kukabidhiwa kadi zao na Kinana (kushoto), katika kata ya Kasanda, Kakonko Kigoma.
Mjumbe wa Shina, Agnes Lukwavi akitoa maoni yake ya kuboresha C CM, wakati Kinana alipozungumza na mabalozi na wazee wa Kata ya Kasanda, wilayani Kakonko, Kigoma

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages