FAMILIA YANUSURIKA KUFA KWA KUGONGWA NA GARI CHUMBANI USIKU WA MANANE
FAMILIA ya mme, mke na mtoto wamenusurika mkoani hapa, baada ya gari
aina ya Noah, kuacha njia na kuwafuata chumbani wakiwa wamelala usiku wa
manane.
Tukio hilo la aina yake, limetokea saa nane usiku wa kuamkia leo,
kwenye chumba cha familia ya Adam Gau kilichopo katika nyumba ya Eliasi
Chebuse, iliyopo kiasi cha mita tano kutoka barabara ya Jamhuri, mjini
Dodoma.
Akizungumzia tukio hilo leo asubuhi, Chiku ambaye ni mke wa Gau alisema,
akiwa amelala na mumewe na mtoto wao mwenye umri wa miaka minne, Muumin
Adam, walisikia kishindo kikubwa kilichoambatana na sehemu kubwa ya
ukuta wa chumba kuporomokea ndani. Pichani askari ambvaye pia ni mkazi
wa nyumba hiyo akionyesha madhara yaliyotokana na chumba kugongwa na
gari. Kushoto ni Mama Gau
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269