Breaking News

Your Ad Spot

Jun 24, 2013

'MUSIC' YA STEVE RNB YAANZA KUTESA



Na Elizabeth John
WAKATI singo yake ya ‘Jambo Jambo’ ‘ikiendelea kufanya vema katika chati mbalimbali za muziki nchini, mkali wa muziki wa bongo fleva, ‘Steve RnB’ ameachia singo mpya inayokwenda kwa jina la ‘Music’, ambayo pia imeanza kutamba katika tasnia hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, mkali huyo alisema ameamua kutoa singo hiyo mpya ili kuendelea kuwapa raha mashabiki wake ambao wamekuwa wakimuunga mkono.
Alisema anayo matumaini makubwa ya wimbo huo kufanya vema katika medani ya muziki wa bongo fleva kama ilivyokuwa kwenye nyimbo zake zilizotangulia.
“Nawashukuru mashabiki kwa kuniunga mkono kwenye kazi zangu, sina cha kuwalipa zaidi ya kuwatayarishia kazi nzuri zaidi ambazo zitawaburudisha na kuwapa mafunzo ndani yake,” alisema.
Steve alipata kutoa singo matata ikiwamo ya ‘One Love’ alioimba na Baby Boy na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages