Breaking News

Your Ad Spot

Jul 16, 2013

DK. BILAL AKUTANA NA WATANZANIA WA ABUDHABI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baadhi ya Watanzani ya waishio mjini Abuja, wakati alipokutana nao katika Makazi ya Ubalozi wa Tanzania Nchini Nigeria, jana Julai 16, 2013 na kufanya nao mazungumzo. Makamu ameondoka leo mjini Abuja kurejea nchini Tanzania, baada ya kuhudhuria Mkutano wa 12 wa siku mbili wa Afrika uliokuwa ukijadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) uliofunguliwa na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan, Julai 15-16, 2013 mjini Abuja Nigeria na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Nchi za Afrika. Kushoto kwake ni mkewe, Mama Asha Bilal. Picha na OMR 

 Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, aliyemaliza muda wake, Siwajibu Baraka Siwajibu, akiwatambulisha baadhi ya Watanzania kwa makamu wa Rais, wakati alipofika kuzungumza nao katika Makazi ya Balozi wa Tanzania, Abuja Nigeria jana Julai 16, 2013. Kushoto ni Mke wa Makamu wa Rais, Mama Asha Bilal, na kutoka (Kulia) ni Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Seif Rashid, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Mahadhi na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Fatma Rajabu. Picha na OMR 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, mkewe Mama Asha Bilal, Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Fatma Rajabu, wakiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya watanzania waishio Abuja, baada ya makamu kufanya nao mazungumzo jana. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mzee, Salu Salatu, ambaye ni raia wa Nigeria aliyefanya kazi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria kwa muda wa Miaka 25 hadi sasa, baada ya Makamu kuzungumza na Watanzania waishio Abuja jana Julai 16, 2013. Makamu ameondoka leo mjini Abuja kurejea Tanzania baada ya kuhudhuria Mkutano wa 12 wa siku mbili wa Afrika uliokuwa ukijadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) uliofunguliwa na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan, Julai 15-16, 2013 mjini Abuja Nigeria na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Nchi za Afrika.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages