Breaking News

Your Ad Spot

Sep 24, 2013

ATHUMANI HAMIS BALOZI WA USALAMA BARABARANI KWA UTHAMINI WA AIRTEL

 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi Airtel (T) ambao wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa mwaka wa tano mfululizo Bi. Beatrice Singano Mallya akisalimiana na  Mwandishi wa Habari Athumani Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na kudhaminiwa na Airtel katika wiki hii ya usalama barabarani mkoani mwanza. Athumani alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini na India.

MWANZA, TANZANIA
 KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu ya Airtel imesema kuwa itahakikisha suala la Usalama barabarani linazingatiwa na jamii ya Watanzania ili kupunguza ajali za barabarani .
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Mallya kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Usalama Barabarani,yanayofanyika Jijini Mwanza.

Alisema kama wadau wa usalama barabarani,wamedhamini maadhimisho hayo ili kuwezesha jamii kupata elimu na uelewa kuhusu matumizi ya barabara,sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani katika kupunguza ajali nchini.

Alisema ajali nyingi nchini zinachelewesha maendeleo na kupunguza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

“Sisi kama wadau tumedhamini maadhimisho haya kwa mwaka wa tano mfululizo,lengo letu tunataka jamii ipate uelewa na hatimaye kupunguza ajali za barabarani zinaoweza kuepukika,ndiyo sababu tuko hapa,” alisema.

Alisema kutokana na kuonesha umahiri wameanzisha mfumo mpya wa ulipiaji  wa leseni za magari kwa kupitia  njia ya Airtel Money.

------
1. usalama barabarani airtel 1
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Emmanuel Nchimbi akisalimiana na
Mwandishi wa Habari Athumani Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na kudhaminiwa na Airtel katika wiki  ya usalama barabarani, mwandishi huyu alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini na India.

1. usalama barabarani airtel 2 na 3
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi
Airtel Tanzania ambao wamekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya wiki
ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa mwaka wa tano mfululizo Bi.
Beatrice Singano Mallya akisalimiana na  Mwandishi wa Habari Athumani
Hamisi ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa Usalama Barabarani na
kudhaminiwa na Airtel katika wiki hii ya usalama barabarani mkoani
mwanza. Athumani alipata ajali ya gari ambayo ilisababisha baadhi ya
viungo vyake kupooza licha ya kupata matibabu nchini Afrika ya Kusini
na India.
 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages