Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuelezea utekelezaji wa majukumu ya Tume hiyo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Agustino Ramadhani. Pamoja na mambo mengine Jaji Warioba amezungumzia namna mikutano ya mabaraza ya katiba iliyoendeshwa kwa ufanisi.
Amesema ili kuendesha mikutano ya katiba kwa ufanisi,Tume ilijigawa katika makundi 14, kila kundi likiwa na wajumbe kati ya wawili na watatu. Makundi haya yalizunguka nchi nzima na kufanya jumla ya mikutano 179 iliyohudhuriwa na wajumbe 19,337. Mikutano hii ilifanyika katika kila Halmashauri ya Wilaya, Halmashaurio ya Manispaa na Jiji na mkutano mmoja ulidumu kwa wastani wa siku tatu. Kati ya mikutano hii, jumla ya mukutano 116 ulifanyika Tanzania Bara na 13 ilifanyika Tanzania Zanzibar.
Your Ad Spot
Sep 26, 2013
Home
Unlabelled
JAJI WARIOBA: MIKUTANO YA MABARAZA YA KATIBA TUMEIFANYA KWA UFANISI MKUBWA
JAJI WARIOBA: MIKUTANO YA MABARAZA YA KATIBA TUMEIFANYA KWA UFANISI MKUBWA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269