Breaking News

Your Ad Spot

Sep 11, 2013

KINANA ATINGA SHINYANGA VIJIJINI LEO


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Mzee wa kata ya Didia .
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kwenye ujenzi wa Birika la kunyweshea mifugo katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na mafundi ujenzi wanaoshiriki kujenga birika la kunyweshea maji mifugo katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa akitoa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa mwananchi aliyeomba kupiga nae picha nje ya soko jipya katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi baada ya kutembelea soko la jipya katika kata ya Didia na kuwapongeza sana wakazi wa kata hiyo kwa kushirikiana na uongozi wake kwa kufanikisha ujenzi wa soko hilo.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amebeba nyoka aina ya chatu nje ya jengo la soko jipya katika kata ya Didia, Nyoka huyo huchezwa kwenye ngoma inayoitwa Wagoyangi.
 Katibu Mkuu akipata maelezo juu ya maendeleo ya ujenzi wa hospitali ktika kata ya Iselamagazi.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa kata ya Iselmagazi wakati wa ziara yake ya wilaya ya Shinyanga Vijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongea na Juma Mayenze mkazi wa kijiji cha Mwasekagi kata ya Solwa ambaye alikuwa anamfikishia ujumbe juu ya tatizo la maji na umeme kijijini hapo.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili uwanja wa mkutano katika kata ya Salawe.

 Wasanii wa kikundi cha Tangawizi wakionyesha sanaa yenye stori nzuri iliyoonekana kufunza uelewa wa hatua za maendeleo ya Mtanzania tangia wakati wa mkoloni mpaka sasa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia umati wa wakati wa kata ya Salawe na maeneoya jirani waliofika kusikiliza sera na misimamo imara ya Chama Cha Mapinduzi.
 Mbunge wa Viti Maalum  Azah Hilal Hamad akihutubia wananchi  kwenye mkutano wa hadhara na kuelezea namna gani serikali sikivu ya CCM inavyojali wananchi wake.
 Mbunge wa Solwa ndugu Ahmed Salum akihutubia wananchi wake na kuelezea namna utekelezaji wa ilani ya uchaguzi unavyoenda vizuri .
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa wilaya ya Shinyanga Vijijini .

 Ngoma ya Kucheza na Fisi ilikuwa na kivutio cha aina yake  katika viwanja vya Salawe.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akikata papai huku Katibu wa NEC Itikadi na Unezi akichukua kipande kingine  cha papai ,Katibu Mkuu pamoja na Katibu wa Uenezi walikuwa kwenye ziara yao ya kujenga na kukiimarisha chama katika  wilaya ya Shinyanga Vijijini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages