Breaking News

Your Ad Spot

Sep 1, 2013

SIXTUS AIDHINIWA KUWA KATIBU MKUU WA UVCCM LEO MJINI ZANZIBAR

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpongeza Katibu Mkuu mpya wa UVCCM Taifa, Sixtus Mapunda baada ya Baraza Kuu la UVCCM kumpitisha rasmi leo Aifisi Kuu ya CCM, Kiswandui Zanzibar.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpongeza Katibu Mkuu mpya wa UVCCM mstaafu, Martine Shigela kwa kumaliza muhula wake wa uongozi, leo Aifisi Kuu ya CCM, Kiswandui Zanzibar.
 Shigela akimkaribisha Sixtus kuchukua nafasi yake meza kuu baada ya Baraza Kuu la UVCCM kumwidhinisha rasi Sixtus leo mjini Zanzibar
 Shigela akimkaribisha Sixtus kuchukua nafasi yake meza kuu baada ya Baraza Kuu la UVCCM kumwidhinisha rasi Sixtus leo mjini Zanzibar. Kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM  Taifa, Sadifa Juma.
 Sixtus akiteta jambo na Mwenyekiti wake
 Shigela akitoa neno la shukurani
 Sixtus akitoa neno la shukurani
  Waalikwa kwenye kikao cha Baraza kuu la UVCCM, lilifanyika leo Kisiwandui, Zanzibar, Katibu wa NEC, Itikasi na Uenezi Nape Nnauye akishauriana jambo na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimi kwenye kikao hicho.
 Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, akifungua Mkutano maalum wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) leo, katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui mjini Zanzibar. Wengine kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Zanzibar), Shaka Abdul Shaka, Katibu  Mkuu wa UVCCM aliyemaliza muda wake, Martine Shigela na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Hamis na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mboni Mhita, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (Katikati) akiwasikiliza, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vuai Ali Vuai na Katibu Mkuu Mstaafu wa UVCCM, Martin Shigela, nje ya Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui mjini Zanzibar kabla ya kikao cha Baraza Kuu kuanza, leo
 Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Mboni Mhita akiselebuka nje ya ukumbi wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la CCM.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Jerry Silaa (kulia) akizungumza na Katibu wa NEC, Itrikadi na Uenezi, Nape Nnauye nye ya Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui mjini Zanzibar kabla ya kikao cha Baraza Kuu la UVCCM kuanza leo. Wengine ni Janurai Makamba, Emmanuel Nchimbi na Shigela
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Ali Seif Iddi akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM, Adulrahman Kinana baada ya kuwasili Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui Zanzibar kufungua kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.
 Wajumbe wa Baraza Kuu la UVCCM, wakiwa nje ya ukumbi wa Kiswandui Zanzibar
 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Ali Seif Iddi akiongoza dua kwenye kaburi la Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, Abeid Amani Karume, Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui, Zanzibar Kabla ya kufungua Mkutano maalum wa Baraza Kuu la UVCCM, leo. Wengine ni kutoka kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Bara)  Mfaume Ally Kizigo, Makamu Mwenyekiti wa UVCCM, Mboni Mhita na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Hamis na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Zanzibar), Katibu Mkuu wa UVCCM Mstaafu, Martine shigela na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.
 Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM kutoka Morogoro, Abubakar Asenga akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati wa mkutano huo
 Martine Shigela akipita kusalimia wajumbe ukumbini baada ya kumaliza muda wake wa uongozi
 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar akiingia ukumbini kufungfungua kikao

 wajumbe ukumbini
Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Bara) akimpongeza Katibu Mkuu mpya Sixtus Mapunda

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages