Breaking News

Your Ad Spot

Nov 2, 2013

KIJANA MIAKA 35 JELA KWA UNYANG'ANYI WA KUTUMIA SILAHA

SIMIYU, Tanzania
Mahakama  ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu imemuhukumu kifungo cha miaka 35 jela kijana Maduhu Magumba (23) mkazi wa bariadi baada ya kupatikana na hatia ya  wizi kwa kutumia silaha.
 
Magumba alikuwa akikabiliwa na kesi ya unyanaganyi kwa kutumia silaha akiwa na kisu pamoja na nondo, akituhumiwa kunyanganya simu pamoja na pesa kiasi cha sh. 362,500, mali ya Seif Ally mkazi wa Bariadi mjini.
 
Awali mwendesha mashtaka wa jeshi la polisi wilayani hapa Samweli Kilabuko alisema mnamo tarehe 26 Agosti mwaka huu saa tano na nusu usiku mshitakiwa aliiba pesa kiasi cha shilingi 362,500 simu moja aina ya nokia yenye dhamani ya shilingi 195,000 jumla ikiwa shilingi 575,500 .
 
Mbali na hiyo kilabuka alieleza kuwa mshitakiwa kabla ya kutenda kosa hilo, alikuwa na kesi mbili katika mahakama ya mwanzo ya Bariadi, akituhumiwa kwa makosa mawili kwanza kutishia kuuwawa, pamoja na na kufanya fujo.
 
Kilabuka aliongeza kuwa katika kesi huizo  mshitakiwa katika kesi ya kwanza alitiwa hatiaani na kufungwa kifungo cha  mwaka mmoja na katika kesi ya pili mshitakiwa alifungwa kifungo cha  miezi 6.
 
Akitoa hukumu  Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Roberti Oguda alisema mahakama kumtia hatiani na kufungwa miaka 35 pamoja na viboko 24, wakati wa kuingi 12 na wakati wa kutoka 12.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages