Breaking News

Your Ad Spot

Nov 29, 2013

KINANA AWASILI MBOZI ASUBUHI HII

 Vijana wa CCM wa Tawi la Mpemba, wilayani Momba, Mbeya, wakiwa na hamu ya kumsalimia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ambaye na msafara wake walikuwa wanakwenda wilayani Mbozi kuendelea na ziara ya kuimarisha chama, kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kusikiliza kero za wananchi.

 Wafuasi wa CCM wakishangilia wakati Katibu wa NEC wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza nao aliposimama kwa muda katika shina la Vijana wa CCM la Mpemba akiwa njiani kwenda wilayani Mbozi, akitokea wilayani Momba.

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na wafuasi wa CCM katika Tawi la CCM la Mpemba, wilayani Momba.

 Kinana akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro alipowasili mjini Mbozi leo.

 Msanii wa kikundi cha ngoma cha Hakuna Kulala, Catherine Kapessa akipuliza baragumu wakati wa mapokezi ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika Ofisi za CCM

 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akiwasalimia baadhi ya viongozi wa CCM msafara wa Kinana ulipowasili Ofisi ya CCM Mbozi leo

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akifurahia ngoma iliyokuwa ikipigwa na wasanii kwenye Ofisi ya CCM Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya leo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages