Breaking News

Your Ad Spot

Dec 16, 2013

WAZIRI MAGHEMBE AKABIDHI VISIMA 20 VILIVYOKARABATIWA NA TBL WILAYANI MISUNGWI

 Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania  (TBL) wa mikoa ya Simiyu, Mwanza  na Mara, Josephat Changwe, akimwongoza Waziri wa Maji , Profesa Jumanne Maghembe (kulia) kuzindua moja ya visima 20 vya maji salama ya kunywa vilivyokarabatiwa na kampuni hiyo kwa gharama ya sh.49.5 milioni, wilayani Misungwi,Mwanza juzi.Anayepiga makofi (kushoto) ni Mbunge wa jimbo la Misungwi, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Charles Kitwanga.
 Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe (kulia), Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais,Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga (wa tatu kulia) na Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania  (TBL) wa mikoa ya Simiyu, Mwanza  na Mara, Josephat Changwe wakisaidia kumtwisha dumu la maji mmoja wa wanawake wa Kijiji cha Mapilinga, Wilaya ya Misungwi, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa moja kati ya visima 20 vilivyokarabatiwa na TBL wilayani humo, kwa sh. mil 49.5.
 Mama akiondoka na maji huku viongozi wakipiga makofi kwa furaha
 Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga (kulia), akipampu maji huku Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe (pili kulia),  na Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa TBL, Steve Kilindo wakionja maji wakati wa hafla ya kukabidhi visima vya maji 20 vilivyokarabatiwa na TBL wilayani Misungwi, Mwanza, kwa sh. mil 49.5, juzi.
  Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa Kampuni ya Bia (TBL),Stephen Kilindo,wa kwanza kulia akitoa taarifa fupi ya ukaratabati wa visima 20 Wilayani Misungwi kwa Waziri wa Maji ,Profesa Jumanne Maghembe wa pili kutoka kushoto.wa pili kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Mariam Lugaila na wa Kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Mapilinga,Benard Busangu juzi
Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, akizungumza na mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Mapilinga Misungwi,baada ya kuzindua kisima cha maji kati ya visima 20 vilivyoakaratbatiwa na Kampuni ya Bia (TBL) kwa sh.49.5 milioni.wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa TBL , Stephen Kilindo na Naibu Waziri Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Misungwi Charles Kitwanga.
Charles Kitwanga (kushoto) akitoa shukrani kwa TBL kwa msaada huo muhimu. PICHA ZOTE NA MDAU BALTAZAR MASHAKA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages