Breaking News

Your Ad Spot

Jan 19, 2014

MAMIA YA WAMZIKA DEUSDEDIT MTAMBALIKE

Jaji Mstaafu Mark Bomani,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye  na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Mh.Stephen Wassira ni miongoni mwa viongozi mbali mbali walioshiriki mazishi ya kada maarufu ambaye pia alishawahi kuwa Mkuu wa Wilaya katika Wilaya mbalimbali nchini.
Mama Anna Mkapa,Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka na Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini Elizabeth Minde wakiwa miongoni mwa mamia ya Watanzania waliojitokeza kumzika kada wa siku nyingi Deusdedit Mtambalike.
Waombolezaji wakiwa kwenye nyuso za huzuni wakati wa mazishi ya mpendwa wao Deusdedit Mtambalike.
Sala ya kumuombea Marehemu Deusdedit Mtambalike aliyefariki tarehe 15 Januari 2014 nchini Afrika ya Kusini ilisomwa nyumbani kwake kabla ya Mazishi.
Wanandugu wa Marehemu Deusdedit Mtambalike wakiwa wamebeba mashada ya maua .
Mwanasiasa wa siku nyingi na ambaye alishawahi kushika nyazfa mbalimbali za serikali Balozi Paul Rupia akitoa salaam za pole kwa familia ya marehemu Deusdedit Mtambalike na kumuelezea marehemu kama mtu aliyemwema na asiyechoka kushauri kwenye jambo lolote alotakiwa kushauri.
Jaji Mstaafu Mark Bomani akimuelezea marehemu Deusdedit kama mtu ambaye hakusita wala kuwa na woga katika kuzungumzia jambo lenye manufaa kwa jamii.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa salaam za rambirambi kwa niaba ya CCM Makao Makuu wakati wa mazishi wa aliyekuwa Kada wa Chama Cha Mapinduzi Marehemu Deusdedit Mtambalike.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Mahusiano na Uratibu) Mheshimiwa Stephen Wassira akitoa salaam za pole kwa niaba ya Serikali kwenye mazishi ya Ndugu Deusdedit Mtambalike yaliofanyika nyumbani kwa marehemu Kimara Bonyokwa.
Watoto wa Marehemu Deusdedit Mtambalike wakiwa wenye nyuso za simanzi na huzuni pamoja na Mama yao na Ndugu wa karibu wakati wa sala ya mwisho kabla ya mazishi ya Baba yao mpendwa.
Sehemu ya watu waliojitokeza kwenye mazishi ya Deusdedit  Mtambalike
Profesa Mahalu akiweka mchanga kama ishara ya kumzika rafiki yake Marehemu Deusdedit Mtambalike
Mke wa Marehemu Deusdedit Mtambalike akiweka shada la maua juu ya kaburi .
Watoto wa marehemu wakiweka shada la Maua kwenye kaburi la baba ya mpendwa Marehemu Deusdedit Mtambalike aliyefariki dunia tarehe 15 Januari 2014 nchini Afrika ya Kusini. Picha zote na Adam Mzee

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages