Breaking News

Your Ad Spot

Mar 19, 2014

KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA AMVAA MKUU WA KITUO CHA POLISI

Na Flora kamaghe Iringa

Katibu wa chama cha mapinduzi  mkoa wa iringa Hassani Mtenga amempa  mda wa wiki moja Mkuu wa Kituo cha polisi mkoani Iringa Siphaeli  Pyuza  kumuomba radhi kwa kitendo cha kwenda kufanya oparesheni ndani ya jengo la Chama Cha Mapinduzi mkoa.

Mtenga (Pichani) alieleza kuwa Pyuza alipita kila chumba bila ustaarabu wowote na kukagua kila chumba kwa madai kuwa  walipewa taarifa kuwa kuna wafuasi wa Chadema waliokuwa wakipigwa na kuteswa  jambo ambalo Mtenga amesema halikuwa la ukweli hivyo walienda kuwahukumu bila kuwa na uhakika wowote.

“tunatoa masikitiko makubwa kwa ocd kuja kutupekua kila chumba ni kitendo cha kutudhalilisha   tunampa mda atuombe radhi isiwe ni sehemu ya kuwasaidia Chadema”


Mbali na hayo  mtenga alitoa ufafanuzi juu ya waraka uliovuja  ambao Chadema walikuwa nao kuwa ulikuwa na sahihi feki ya katibu mkuu mwigulu nchemba,waraka huo ulikuwa ukitoa ufafanuzi juu ya fedha ambazo zimetolewa kwa Chama Cha Mapinduzi kwaajili ya uchaguzi wa ubunge jimbo la kalenga.

Kwa madai ya chadema walieleza kuwa fedha hizo zilionesha kuwa waalitumia rushwa kwa wananchi ili kuweza kupata ushindi mkubwa wa jimbo la Kalenga kuweza kuchukuliwa na Chama Cha Mapinduzi kwani barua waliokuwa nayo ilionesha  matumizi ya fedha hizo lakini katibu alikanusha suala hilo.

Hassan alieleza kuwa hizo ni fitina tu za chama cha demokrasia na maendeleo ambazo wanatumia kwaajili ya kuwachokonoa chama cha mapinduzi na alisema kuwa chadema wanapaswa kuwa na akili kwani mambo wanayofanya ni kukidhalilisha chama chao

Hata hivyo Hassani alisema  kuwa  CHADEMA wamekuwa wakimfuatilia  kwa mda mrefu na aliwataka  ugomvi wao wa kisiasa ufikie katika majukwaa na sio kila kosa kukimbilia polisi  kwaajili ya kumtafutia mtu sababu ya kumkamata.

“Chadema wanasema kuwa mimi nikikamatwa na polisi watafurahi sana wananitafutia mimi kosa la kukamatwa kwasababu gani ugomvi wetu uishie majukwaani sio polis alisema mtenga”


Hata hivyo Mtenga  amewataka wanachama wake kuendelea kuwa na mshikamano  na waweze kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi na kuendelea kudumisha amani iliyopo katika nchi isiweze kuvunjwa na mtu yeyote na endapo yeyote atakaekamatwa kushinikiza au kuvunja amani hatua kali zitachukuliwa dhidi yake

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages