Breaking News

Your Ad Spot

Mar 8, 2014

MAMA ADAIWA KUTOWEKA NA MTOTO ANAYEHITAJI MSAADA

Katika hali ya Kutatanisha na kushangaza mama mkubwa wa Mtoto aliye ungua moto na kusababisha shingo yake kuungana na mwili ametoweka na mtoto huyo huku wasamalia wema waliokuwa wakiendelea kutoa michango yao kwa ajili ya kumsaidia akatibiwe wakiwa wanaendelea kufanya hivyo.

Mama huyo alitoweka mapema alfajili jana huku asiseme ni sehemu gani alikuwa amekwenda bila hata kuaga kwa mtu yeyote yule, Kutokana na swala hili Tulikuwa tunaomba wale watu wote wanao endelea kumchangia mtoto huyo na wanaopanga kumchangia kupitia namba hii ya mama huyo  0752 986879 wasitishe kufanya hivyo, na mpaka sasa namba yake haipatikani na taratibu za kumsaka zinaendelea.
Tutaendelea kuwafahamisha..
Huyu ndiye Mama Mkubwa wa Mtoto Adolotea Nyavike bi. Salome Kiegu (35) ambaye ametoweka na mtoto huyo kusiko julikana huku wasamalia wema wakitaka kutoa misaada.
Mtoto Adolotea Njavike(1.4) ambae Kichwa na Kiwiliwili vimeungana baada ya kupata na ajali ya Moto akiwa na mama yake Mzazi. Na mbeya yetu

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages