Breaking News

Your Ad Spot

Mar 27, 2014

RIDHIWANI ANAFAHAMU WANANCHI WAKE NA CHANGAMOTO ZAO

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimnadi mgombea wa nafasi ya ubunge jimbo la Chalinze  kupitia CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye kijiji cha Mazizi ambapo alisema moja ya sifa za mgombea ni kuwafahamu wananchi wake, na wananchi wake kumfahamu, kufahamu changamoto za wananchi na kufahamu namna ya kuzitatua changamoto hizo.
 Ridhiwani Kikwete akijinadi kwa wananchi wa kijiji cha Mazizi kata ya Msata ambapo aliahidi kujenga shule,kusaidia wakina mama na vijana,kushirikiana na wana Chalinze katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya afya,kuinua kilimo,kufanya juhudi za dhati kuboresha kilimo.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Ridhiwani Kikwete  akifungua shina la Tonga Road wakati  wa ziara za mikutano ya  kampeni za ubunge.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Tonga wakati wa kumnadi mgombea wa CCM jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete.
 Wazee wa kijiji cha Diozile wakisoma vipeperushi vyenye wasifu wa Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge jimbo la Chalinze zilizofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Lubaya.
 Kila aina ya furaha kwa vijana wa Msoga ambapo mgombea wa Ubunge jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete alifanya mkutano wa hadhara kwa wananchi wa kijiji hicho.
 Karibu wa NEC Itikadi na Uenezi akihutubia wapiga kura wa Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Msoga ambapo wananchi hao wamesema kijijini kwao hakutokuwa na kura kwa wapinzani.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Ridhiwani Kikwete akikata utepe kufungua shina la UVCCM Msoga baada ya kumaliza mkutano wa hadhara wa kampeni za ubunge.

MGOMBEA UBUNGE KUPITIA CUF LAWAMANI CHALINZE


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye akizungumza na Mwenyekiti wa UWT Kata ya Ubena Jesca Daudi ambaye alivunjwa mkono na Viongozi wa CUF waliovamia ofisi ya kata kwenye kijiji cha Tokamisasa.
 Katibu wa Wilaya ya Makete Miraji Mtaturu akizungumzia tukio lililomkuta  Mwenyekiti wa UWT Kata ya Ubena Jesca Daudi ambaye alivunjwa mkono na Viongozi wa CUF waliovamia ofisi ya kata kwenye kijiji cha Tokamisasa kuwa ni kitendo cha kinyama na cha kupingwa kwa nguvu zote na kitendo hicho kimemvua sifa za kuwa mgombea ubunge  wa CUF.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages