Breaking News

Your Ad Spot

Mar 26, 2014

WAJERUMANI KUSAIDIA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UJANGILI, SERIKALI YA UJERUMANI KUTUMIA EURO MILIONI 10 KUKARABATI RELI YA KATI

DSC_0080
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Dkt. Frank Steinmeier akizungumza waandishi wa habari kwenye mkutano huo jijini Dar es Salaam na kuelezea mafanikio ya ushirikiano wa nchi hizo mbili. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe.(Picha na Zainul Mzige).
Na Damas Makangale, MOblog
HUKU Tembo wakiendelea kuuawa katika mbuga kadhaa nchini, Serikali ya Ujerumani imeahidi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kupambana tatizo la ujangili Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe Bernard Membe amesema serikali ya ujerumani imeahidi kutoa msaada wa vifaa na ujuzi wa kupambana na ujangili katik mbuga za Tanzania.
“tupo katika hatua za mwisho za ushirikiano wa kupambana ujangili na majangili ili kunusuru Tembo wetu kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo,” amesema Membe.
Waziri Membe amesema kwamba serikali ya Ujerumani imetoa magari ya kupambana ujangili, camera, vifaa vya kisasa na mafunzo kwa askari wa wanyamapori ili kuwajengea uwezo wa kupambana na majangili nchini.
DSC_0048
Picha juu na chini ni Baadhi ya wageni waalikwa na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wa Ujerumani nchini.
Amesema tatizo la ujangili si la Tanzania peke yake linahitaji ushirikiano na nchi mbalimbali za Afrika na ulaya kwa sababu pembe za ndovu kuuzwa kwenye nchi hizo au kuwa kama njia ya kupitishia.
“wanatoa mafunzo ya kutosha kwa askari wetu wa wanyamapori ili waweze kukabiliana kikamilifu na majangili,” aliongeza
Waziri Membe alizungumza kwenye mkutano wa pamoja na Waziri wa Mambo ya nchi za Nje wa Ujerumani Dkt Frank-Walter Steinmeier ambaye alitembelea nchini kwa mara ya kwanza tangu kushika nyadhifa hiyo
Kwa taarifa ambazo zipo ni kwamba Tembo 25,000 waliuawa mwaka 2011 na 22,000 waliuawa mwaka 2012, ni ishara inayoonyesha kuwa biashara haramu ya wanyama pori sasa imekuwa ni uhalifu wa kidunia wenye nguvu ya kuathiri maendeleo ya kiuchumi, kusababisha migogoro, kuimarisha vikundi vya kigaidi na kuathiri watu wenye hali duni ya watu waishio katika umaskini.
Faru wanauawa na maharamia kila baada ya dakika 10 na ni wachache kuliko chui 3,500 ambao wamebaki porini.
Ujangili unaathiri jamii barani Afrika, hususan yale maeneo katika bara ambapo wanakabiliwa na hali mbaya ya janga la ujangili.
DSC_0054
DSC_0045
Sehemu ya waandishi wa habari nchini pamoja na waandishi kutoka nje ya nchi waliohudhuria mkutano huo jijini Dar.
DSC_0001
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe Bernard Membe na mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani nchini, Dkt Frank-Walter Steinmeier wakiwasili kwenye chumba cha mkutano kuzungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar.(Picha na Zainul Mzige wa MObog).
Na Damas Makangale, MOblog Tanzania
SERIKALI ya Ujerumani kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania imeahidi kutumia zaidi ya Euro milioni 10 kukarabati reli ya kati (Central Line Railway). MOblog inaripoti.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasili kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani nchini, Dkt Frank-Walter Steinmeier, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe Bernard Membe amesema serikali ya Ujerumani imekubali kwa dhati kabisa kukarabati reli ya kati kwa manufaa ya Tanzania na nchi jirani.
“kwa sasa siwezi kusema ukarabati utaanza lini na jina la mwekezaji kwa sababu mazungumzo yanaendelea lakini kwa hakika kabisa tumeshakubaliana kwenye jambo la ukarabati wa reli ya kati,” amesema Waziri Membe
Amesema reli ya kati itapunguza matumizi ya barabara kwa mizigo na barabara za nchi zitakuwa salama na kuongeza tija katika Nyanja za biashara kupitia soko la pamoja Afrika Mashariki na kati.
DSC_0072
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Dkt. Frank Steinmeier akizungumza waandishi wa habari kwenye mkutano huo jijini Dar es Salaam na kuelezea mafanikio ya ushirikiano wa nchi hizo mbili.
Membe alilisisitiza kwamba ziara ya Waziri mpya wa mambo ya nje kutoka Ujerumani ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa sababu amekuja na wawekezaji 65 kutoka maeneo mbalimbali.
Amesema kuwa ukarabati wa reli ya kati ni muhimu katika kudumisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizo mbili kwa maslahi ya watu wao.
“reli ya kati kama mnavyojua ilijengwa na Wajerumani mwaka 1913 na kwa sasa ina miaka karibu mia moja na kitu,” aliongeza Waziri Membe
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Dkt. Steinmeier amesema kuwa nchi yake itaendelea kudumisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii na Tanzania katika jitihada za kuharakisha maendeleo ya nchi na watu wake.
Amesema kuwa serikali ya Ujerumani imeamua kukarabati reli ya kati katika jitihada za kukumbuka na kudumisha historia ya muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.
“najisikia furaha na faraja kuona nchi yaTanzania inapiga hatua mbele kimaendeleo baada ya uhuru wake,” amesema
DSC_0096
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushirikiano wa kihistoria na kiuchumi kati ya Tanzania na Ujerumani jijini Dar es Salaam.
DSC_0112
Baadhi ya wageni waalikwa na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wa Ujerumani nchini.
DSC_0043
Sehemu ya waandishi wa habari nchini pamoja na waandishi kutoka nje ya nchi waliohudhuria mkutano huo leo jijini Dar.
DSC_0116
Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima akiuliza swali wakati wa mkutano huo.
DSC_0122
Waziri Membe na mgeni wake wakiondoka kwenye chumba cha mkutano kuelekea Ikulu kuonana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages