Breaking News

Your Ad Spot

May 10, 2014

KINANA AFUNIKA NZEGA, KIGWANGALA NA BASHE WACHUANA KUTOA MISAADA MBELE YAKE

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wananchi mkutano wa hadhara uliofanyika leo Mei 10, 2014, kwenye  Uwanja wa Parking mjini Nzega, akiwa katika ziara ya kukagua uhai wa Chama, kukagua utekelezaji wa ilani ya chama na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia ya kuzitatua mkoani Tabora.

Kinana akimsikiliza Samson Mabula aliyekuwa akieleza kero za wachimbaji wadogo, kwenye mkutano huo wa hadhara wa Parking, Nzega.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akihutubia katika  mkutano huo uliofanyika Uwanja wa Parking mjini Nzega
Nape akipokea mabango ya wananchi waliotaka kero zao zisikilizwe na Kinana kwenye mkutano huo wa vianja vya Parking, Nzega.
 Mkuu wa mkoa wa Tabora Fatma Mwasa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye mkutano huo

Mbunge wa Nzega, Hamisi Kigwangala akihutubia kwenye mkutano huo wa hadhara  uliofanyika viwanja vya  Parking, Nzega mkoani Tabora.
Bango kwenye mkutano huo wa hadhara wa CCM mjini Nzega.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisikiliza ushauri kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Tabora, Fatma Mwassa, wakiwa meza kuu kwenye mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisoma mabango kwenye mkutano huo wa kwenye viwanja vya Parking mjini Nzega.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikabidhi mashine ya kutotolea vifaranga kwa wajasiriamali Nzega wakati wa mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Nzega, Hamis Kigangala ambaye ametoa msaada wa mashine hiyo.Kinana akimkabidhi katibu wa UWT Nzega, Arafa Njechele pikipiki kwa ajili ya shughuli za jumuia hiyo ya chama. Pikipiki hiyo pamoja na nyingine  mbili zilizotolwa kwa ajumuia za UVCCM na Wazazi, vimetolewa na mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM, Hussein Bashe (kulia).
Kinana akimkabidhi sh. milioni 2, kiongozi wa Vikundi vya Mamalishe wa  Nzega, Mary Igogo wakati wa mkutano huo. Fedha hizo zimetolewa na Bashe (kulia).
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akihutubia mkutano wa hadhara katika Kata ya Ndala, leo Mei 10, 2014
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akishiriki ujenzi ofisi ya CCM  Kata ya Nkiniziwa, Nzega, Mei 10, 2014
Bashe akimkabidhi Kingwangala sh. 500,000 ambazo alitoa kwa katibu Mkuu wa CCM, Kinana (wapili kushoto), leo, Mei 10, 2014, kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya CCM tawi la Kipugala, jimbo la Nzega ambalo mbunge wake ni Kigwangala.
 Kinana akizungumza baada ya kukagua maabara ya sekondari ya Kampala Kata ya Ndala wilayani Nzega. (Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages