Mmiliki wa Manchester United mmarekani Malcom Glazer ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 85 .
Familia
ya bwenyenye huyo ilinunua United kwa gharama ya Euro milioni 790 mnamo
mwezi Mei mwaka wa 2005 licha ya pingamizi kali kutoka a kwa mashabiki
wa klabu hiyo.
Hata
hivyo, Chini ya umiliki wake uliosabibisha deni kubwa kwa klabu hiyo
''the Red Devils'' walishinda taji la premia ya Uingereza mara tano na
vile vile taji la klabu bingwa mwaka wa 2008 .
Wanawe
mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote
wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa
wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuadhiri umiliki wa United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo .
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenyehisa katika soko la hisa la NY stock Exchange.
Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl .
Bwenyenye
huyo ambaye hakuwahi kanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya
kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga
njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.
Glazer
inasemekana alianza kisiriri kuwashawishi wenye hisa wa klabu hicho
kumuuzia hisa zao tangu mwaka wa 2003 kabla ya kutwaa umiliki wama wa
2005.
United
ambayo msimu uliopita ilitangaza faida kubwa ya asilimia 20 yaani pauni
milioni 418 inakabiliwa na deni la zaidi ya pauni milioni 400.
Glazer aliyeugua kiharusi tangu mwaka wa 2006 amewawachia wanawe sita umiliki wa klabu hiyo ya Uingereza.Chanzo BBC
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269