Breaking News

Your Ad Spot

May 31, 2014

PICHA KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS-IKULU:MAKAMU WA RAIS DKT. BILA AFUNGUA MKUTANO WA TATU WA BARAZA LA MAWAZIRI WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU NA NCHI MAJIRANI ZA UMOJA WA KUDHIBITI SILAHA NDOGO (RECSA).

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima, akizungumza wakati wa mkutano huo kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais kufungua mkutano huo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Mkutano Maalum wa tatu wa Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Nchi Majirani zinazounda Umoja wa kudhibiti Silaha ndogo (RECSA), uliofanyika leo mchana kwenye Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam. Umoja huo unaundwa na nchi 15 ambazo  ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Shelisheli, ElitreaAfrika ya Kusini, Jibuti na Afrika ya Kati.
  Baadhi ya wadau na washiriki wa mkutano huo, wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia kwenye ufunguzi wa Mkutano huo leo kwenye Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages