Tanzania
kwa mara ya Kwanza imesema inayo uhakika kuwa waasi wa M23
walioondolewa nchini Jamuhuri ya Kongo ni ni raia Rwanda.Waziri wa Mambo
ya Nje wa nchi hiyo Benard Membe ameliambia Bunge la Tanzania kuwa anao
uhakika kuwa waasi M23 walitokea nchini Rwanda.
Hii ni Mara kwanza kwa Tanzania kukiri hadharani kuwa inao uhakika kuwa waasi hao ni raia wa RwandaTanzania
ni miongoni mwa nchi ambazo zimepeleka majeshi Jamuhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo ambayo kwa kushirikiana na yale ya umoja wa Mataifa
yaliwaondoa waasi hao DRC
Matamshi
hayo ya Waziri huyo aliyatoa wakati alipokuwa akiwasilisha hotuba ya
Bajeti ya Wizara yake ambapo pia alikiri kuwa bado uhusiano wa Tanzania
na Rwanda sio mzuri.
Hata
hivyo upande wa Upinzani mlishambulia Waziri huyo wa Mambo ya nje Benard
Membe wakidai kwamba Waziri huyo anachochea kuvurugika kwa uhusiano wa
Watanzania na Rwanda kwa kuhisi kuwa M23 ni Wanyarwanda nahata kutaka
achukuliwe adhabu kali.
Mbali
na tuhuma hizo Waziri Membe alizidi kusisitiza kuwa waasi wa M23 ni raia
wa Rwanda akisema hiyo ni ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Mbali na waziri baadhi ya wabunge wanamuunga mkono waziri Membe kuwa waasi wa M23 ni raia wa Rwanda wao.
Matamshi
haya Waziri wa Tanzania kuhusu M23 bado haijulikana ni kwa namna gani
utaathiri uhusiano wa Tanzania na Rwanda kama utakuwepo huenda
ukajulikana hapo baadae.Chanzo BBC Swahili
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269